Maelezo ya Chini
a Hata mwanamume mwaminifu Ayubu alikengeuka sifa yake iliposhambuliwa na marafiki wake watatu. Mwanzoni, alipopoteza watoto wake na mali zake zote, “Ayubu hakutenda dhambi wala hakumlaumu Mungu kwa kutenda jambo lolote baya.” (Ayu. 1:22; 2:10) Hata hivyo, Ayubu aliposhtakiwa kwamba alikuwa ametenda dhambi, alianza ‘kuzungumza ovyoovyo.’ Alikazia fikira kutetea sifa yake mwenyewe badala ya kulitakasa jina la Mungu au sifa yake.—Ayu. 6:3; 13:4, 5; 32:2; 34:5.