Maelezo ya Chini
c Hatimaye, Mahakama Kuu iliamua kwamba akina ndugu warudishiwe kiwanja chao ambapo Betheli ilikuwa imeanza kujengwa mwanzoni mwa miaka ya 1980. Baadaye wanajeshi waliishi kwenye kiwanja hicho. Hata hivyo, wanajeshi walipoondoka hatimaye mwaka wa 2000, wakuu wa eneo hilo waligawanya kiwanja hicho visehemu-visehemu na kuwauzia maskwota kwa njia haramu. Sasa mamia ya maskwota wanaishi kwenye kiwanja hicho. Tatizo hilo bado halijasuluhishwa.