Maelezo ya Chini
b Kwa mfano, karibu na mwaka wa 785 W.K., Charlemagne alitoa amri iliyosema kwamba mtu yeyote katika eneo la Wasaksoni ambaye angekataa kubatizwa na kuwa Mkristo angeuawa. Pia, mkataba wa Amani ya Augsburg, uliotiwa sahihi mnamo 1555 W.K. na vikundi vilivyokuwa vikipigana vya Milki Takatifu ya Roma, ulisema kwamba kila mtawala katika eneo lililo ya chini milki hiyo alipaswa kuwa Mkatoliki au Mlutheri na kwamba kila mtu aliye chini ya utawala wake alipaswa kukubali dini ya mtawala huyo. Wale waliokataa kujipatanisha na dini ya mtawala huyo walilazimishwa kuhama.