Maelezo ya Chini
a Katika Biblia, maneno ya awali yaliyotafsiriwa “fidia” yanatoa wazo la bei, au kitu chenye thamani, kinacholipwa. Kwa mfano, kitenzi cha Kiebrania ka·pharʹ kimsingi kinamaanisha “funiko.” (Mwanzo 6:14) Kwa kawaida kinamaanisha kufunika dhambi. (Zaburi 65:3) Nomino inayopatana na neno hilo koʹpher inawakilisha bei iliyolipwa ili kutimiza tendo hilo la kufunika, au kukomboa. (Kutoka 21:30) Vivyo hivyo, neno la Kigiriki lyʹtron, ambalo kawaida hutafsiriwa kuwa “fidia,” pia, linaweza kuwa “bei ya ukombozi.” (Matthew 20:28; The New Testament in Modern Speech, ya R. F. Weymouth) Waandikaji wa Kigiriki walitumia neno hilo kumaanisha malipo yanayotolewa kumkomboa mtu aliyetekwa nyara vitani au kumwachilia huru mtumwa.