Maelezo ya Chini
a Imani katika kutokufa kwa nafsi na kuzaliwa upya katika mwili mwingine ni imani ambazo inaonekana zilianzia Babiloni la kale. Baadaye, wanafalsafa Wahindi walianzisha fundisho la Karma. Kulingana na kitabu Britannica Encyclopedia of World Religions, Karma ni “sheria ya kisababishi na tokeo, ambayo inasema kwamba mambo ambayo mtu anafanya katika maisha ya sasa atapata matokeo yake katika maisha yake yanayofuata.”—Ukurasa wa 913.