Maelezo ya Chini
a Tafsiri fulani za Biblia zinatumia neno “Lusifero” kwenye Isaya 14:12, jina ambalo watu fulani wanasema kuwa ni jina la malaika aliyekuja kuwa Shetani Ibilisi. Hata hivyo, neno la awali la Kiebrania lililotumiwa katika mstari huo linamaanisha “mwenye kung’aa.” Muktadha unaonyesha kwamba neno hili linawakilisha, si Shetani, lakini utawala wa Babiloni ambao Mungu alisema angeunyenyekeza kwa sababu ya kiburi chake. (Isaya 14:4, 13-20) Maneno “mwenye kung’aa” yalitumiwa kudhihaki utawala wa Babiloni baada ya kuangushwa.