Maelezo ya Chini
e Unabii huu unapatikana katika kitabu cha Zekaria, hata hivyo, mwandikaji wa Biblia Mathayo alisema kwamba ‘ulisemwa kupitia nabii Yeremia.’ (Mathayo 27:9) Inaonekana kwamba nyakati nyingine kitabu cha Yeremia kiliwekwa kwanza katika sehemu ya Maandiko iliyoitwa “Manabii.” (Luka 24:44) Inaonekana kwamba Mathayo alitaja “Yeremia” kurejelea mkusanyo huo wote wa vitabu, uliotia ndani kitabu cha Zekaria.