Maelezo ya Chini
b Watu fulani wanapinga matumizi ya neno “Mwana wa Mungu,” wakiamini kwamba inamaanisha Mungu alifanya ngono na mwanamke. Hata hivyo, wazo hilo halifundishwi katika Maandiko. Badala yake, Biblia inamwita Yesu “Mwana wa Mungu” na “mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote” kwa sababu yeye ndiye aliyeumbwa kwanza na yeye tu ndiye aliyeumbwa moja kwa moja na Mungu. (Wakolosai 1:13-15) Biblia pia inamtaja mwanadamu wa kwanza, Adamu, kuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Anaitwa hivyo kwa sababu Adamu aliumbwa na Mungu.