Maelezo ya Chini
c Kulingana na toleo la funzo la NIV (NIV Study Bible), jina la Mungu limerudiwa-rudiwa katika mistari hii “ili kukazia maana na pia kuongeza uzito kwenye maneno yaliyo kwenye [mstari wa 27].” Hata hivyo, baadhi ya watu wanadai kwamba kurudiwa mara tatu kwa jina la Mungu katika mistari hiyo kunaunga mkono wazo la kwamba Mungu ni Utatu. Hilo si kweli. Kitabu kimoja kinachofafanua Biblia ambacho kinaunga mkono Utatu kinasema wazi kwamba kutumiwa kwa jina la Mungu mara tatu hapa “hakungempa kuhani aliyetoa baraka wazo hilo, wala watu waliopokea baraka hiyo hawangepata wazo hilo. Kwa maoni yao, kurudia jina la Mungu mara tatu kuliongeza ubora wa baraka hiyo na kuifanya iwe kamili.” (The Pulpit Commentary, Buku la 2, ukurasa wa 52) Kwa habari zaidi, ona makala “Je, Fundisho la Utatu Liko Katika Biblia?”