-
Shabaha ya Mashambulizi ya SovietiAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
wakihubiri kwa bidii katika Muungano wa Sovieti. Huko Estonia mashambulizi yalianza mwezi wa Agosti mwaka wa 1948 wakati wasimamizi watano wa kazi hiyo walipokamatwa na kufungwa gerezani. “Muda si muda ikawa dhahiri kwamba wapelelezi wa KGB walinuia kuwakamata Mashahidi wote,” akasema Lembit Toom, Shahidi wa Estonia. Mashahidi wote katika Muungano wa Sovieti walikabili hali hiyohiyo.
Viongozi wa Sovieti waliwataja Mashahidi kuwa wahalifu wabaya sana na kwamba wao ni tisho kwa Serikali ya Sovieti isiyoamini kuwapo kwa Mungu. Kwa hiyo, walisakwa kila mahali, wakakamatwa, na kufungwa gerezani. Kichapo The Sword and the Shield kilisema hivi: “Wasiwasi mkubwa ambao maofisa wakuu wa KGB walikuwa nao kuelekea Mashahidi wa Yehova unaonyesha waziwazi jinsi walivyowachukia watu waliokuwa na maoni tofauti.”
Wasiwasi wao ulidhihirishwa wakati waliposhambulia Mashahidi mnamo mwezi wa Aprili 1951. Miaka miwili tu iliyopita, mnamo mwaka wa 1999, Profesa Sergei Ivanenko, msomi Mrusi anayeheshimiwa, alisema katika kitabu chake The People Who Are Never Without Their Bibles kwamba mapema mwezi wa Aprili 1951, “familia zaidi ya 5,000 za Mashahidi wa Yehova kutoka jamhuri za Sovieti za Ukrainia, Belorusia, Moldavia, na Baltiki zilihamishwa hadi ‘makao ya kudumu’ huko Siberia, Mashariki ya Mbali, na Kazakhstan.”
Tukio Linalostahili Kukumbukwa
Hebu wazia jitihada zilizohusika katika shambulizi hilo—kukusanya maelfu ya familia za Mashahidi kutoka kwenye eneo kubwa hivyo kwa siku moja tu? Wazia kukusanya mamia, ama maelfu ya watu, ili wafanye kazi ya kutambulisha Mashahidi, kisha kuvamia ghafula nyumba zao zote usiku mmoja. Halafu, kulikuwa na kazi ya kupakia watu kwenye mikokoteni, magari yanayokokotwa na wanyama, na magari mengine. Kisha kuwapeleka kwenye vituo vya magari ya moshi, na kuwapakia kwenye mabehewa ya mizigo.
Fikiria pia mateso yao. Je, waweza kuwazia pia jinsi walivyolazimishwa kusafiri kwa maelfu ya kilometa—kwa muda wa majuma matatu au zaidi, huku wakiwa kwenye mabehewa machafu, yaliyosongamana watu ambayo hayakuwa na vyoo ila ndoo ya kujisaidia tu? Jaribu kuwazia ukiachwa tu kwenye nyika ya Siberia. Nawe wafahamu kwamba si rahisi kuishi kwenye mazingira hayo magumu.
Mwezi huu ni ukumbusho wa miaka 50 tangu kuhamishwa kwa Mashahidi wa Yehova mnamo Aprili mwaka wa 1951. Masimulizi ya wale waliookoka ambayo yamerekodiwa kwenye ukanda wa vidio yanaonyesha jinsi walivyodumisha uaminifu licha ya kuteswa kwa miaka mingi. Masimulizi hayo yaonyesha kwamba jitihada za kuzuia watu kumwabudu Mungu haziwezi kufaulu. Hata Wakristo wa karne ya kwanza hawakuacha licha ya vizuizi.
Matokeo ya Uhamisho Huo
Serikali ya Sovieti iligundua upesi kwamba kuzuia Mashahidi kumwabudu Yehova hakukuwa kazi rahisi kama ilivyodhaniwa. Bila kujali malalamiko makali ya askari, Mashahidi walimwimbia Yehova sifa walipokuwa wakipelekwa uhamishoni. Waliangika ishara zilizosema hivi kwenye mabehewa yaliyowabeba: “Mashahidi wa Yehova Garini.” Shahidi mmoja alieleza hivi: “Tulipokuwa njiani tulikutana na magari mengine ya moshi vituoni, yaliyobeba wahamishwa, nasi tuliona ishara zilizoangikwa kwenye mabehewa.” Tulitiwa moyo kama nini!
Kwa hiyo badala ya kuvunjika moyo, wale waliokuwa wakihamishwa walidhihirisha roho kama ya mitume wa Yesu. Biblia yasema kwamba baada ya kupigwa viboko na kuagizwa wakome kuhubiri, ‘waliendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo.’ (Matendo 5:40-42) Kwa kweli, ni kama Kolarz alivyosema kuhusu uhamisho huo, “haukuwa mwisho wa ‘Mashahidi’ nchini Urusi, ila ulikuwa mwanzo tu wa kazi yao ya kuwahubiria wengi. Hata walijaribu kuwahubiria watu vituoni wakiwa njiani kuelekea uhamishoni.”
Mashahidi walipowasili sehemu mbalimbali, walisifiwa kuwa wafanyakazi watiifu na wenye bidii. Lakini, kama mitume wa Kristo, ni kana kwamba waliwaambia wale waliowanyanyasa: ‘Hatuwezi kukoma kusema juu ya Mungu wetu.’ (Matendo 4:20) Wengi walisikiliza mafundisho ya Mashahidi na kujiunga nao kumtumikia Mungu.
Kolarz aeleza matokeo: “Serikali ya Sovieti ilipowahamisha ilisaidia sana kusambazwa kwa dini yao. ‘Mashahidi’ walihamishwa kutoka kwenye vijiji vyao vilivyojitenga [katika jamhuri za magharibi mwa Sovieti] na kupelekwa sehemu mbalimbali zenye watu wengi, kwenye kambi za mateso au za kazi ngumu.”
Jitihada za Kukabiliana na Ongezeko
Viongozi wa Sovieti walijaribu mbinu mbalimbali ili kukomesha kazi ya Mashahidi wa Yehova. Walianzisha mpango madhubuti wa kueneza habari za uwongo kuhusu Mashahidi, kwa kuwa mnyanyaso mkali haukufaulu. Walitumia vitabu, filamu, na vipindi vya redio. Wapelelezi waliozoezwa wa KGB walijiunga na makutaniko kisirisiri.
Habari za uwongo zilizoenezwa kote ziliwafanya watu wengi wahofu na kutowaamini Mashahidi bila sababu, hilo lathibitishwa na makala moja katika kitabu Reader’s Digest cha Agosti 1982, Chapa ya Kanada. Makala hiyo iliandikwa na Vladimir Bukovsky, Mrusi aliyeruhusiwa kuhamia Uingereza mwaka wa 1976. Aliandika hivi: “Jioni moja niliona ubao kwenye jengo moja jijini London uliotangaza hivi: MASHAHIDI WA YEHOVA . . . Sikuweza kuendelea kusoma, nilipigwa na bumbuazi na kushtuka sana.”
Vladimir aeleza kilichomfanya ahofu: “Haya ndiyo madhehebu ambayo wenye mamlaka nchini mwetu huita mahayawani katili ili kuwaogopesha watoto . . . Katika Muungano wa Sovieti, ‘Mashahidi’ wako gerezani na kwenye kambi za mateso tu. Na sasa nilisimama mbele ya jengo na kutazama ubao wenye jina lao. Je, kweli mtu yeyote angeweza kuwatembelea tu kirafiki?” akauliza. Ili kukazia sababu iliyomfanya ahofu, Vladimir alimalizia kwa kusema hivi: “‘Mashahidi’ wanasakwa sana katika nchi yetu kama vile wahuni wa Mafia wanavyosakwa Uingereza, nao hawaeleweki hata kidogo.”
Lakini Mashahidi walivumilia na kuongezeka sana licha ya mnyanyaso mkali na uenezaji wa habari za uwongo kuwahusu. Vitabu vya Sovieti kama vile The Truths About Jehovah’s Witnesses, kilichochapishwa kwa nakala 100,000 za Kirusi, katika mwaka wa 1978, kilidokeza kwamba habari za uwongo zinazokashifu Mashahidi zinahitaji kuenezwa kwa mapana na marefu. Mtungaji wa kitabu hicho, V. V. Konik, ambaye alieleza jinsi Mashahidi walivyokuwa wakihubiri wajapozuiwa, alishauri hivi: “Wasovieti wanaochunguza dini wanapaswa kubuni njia bora zaidi za kukomesha mafundisho ya mashahidi wa Yehova.”
Mbona Wakawa Shabaha ya Mashambulizi?
Kwa ufupi, Mashahidi wa Yehova walikuwa shabaha kuu ya mashambulizi ya Sovieti kwa sababu waliwaiga wafuasi wa mapema wa Yesu. Katika karne ya kwanza, mitume waliagizwa ‘wasifulize kufundisha juu ya msingi wa jina [la Yesu].’ Hata hivyo, wale waliowashtaki walilalamika hivi baadaye: “Tazameni! mmejaza Yerusalemu fundisho lenu.” Mitume hawakukana kwamba walikuwa wakihubiri wajapokatazwa, badala yake walijibu hivi kwa heshima: “Lazima sisi tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”—Matendo 5:27-29.
Mashahidi wa Yehova leo huchukua kwa uzito
-
-
Jinsi Dini Ilivyookoka MashambuliziAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 8, 9]
-