-
Kuwasiliana na PepoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
na kuwasiliana na pepo au kutii sheria zozote za mtu mwenye kuwasiliana na pepo.)
Vaa “mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu” ambayo yanafafanuliwa katika Waefeso 6:10-18 na uwe na bidii katika kuyadumisha yote katika hali nzuri.
-
-
Kuzaliwa Mara ya PiliKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuzaliwa Mara ya Pili
Maana: Kuzaliwa mara ya pili kunahusisha kubatizwa katika maji (‘kuzaliwa kwa maji’) na kuzaliwa kwa roho ya Mungu, kwa njia hiyo kuwa mwana wa Mungu mwenye tumaini la kutawala katika Ufalme wa Mungu. (Yoh. 3:3-5) Yesu alizaliwa mara ya pili, hali kadhalika wale 144,000 walio warithi pamoja naye wa Ufalme wa mbinguni.
Kwa nini ni lazima Wakristo fulani ‘wazaliwe mara ya pili’?
Mungu amekusudia kushirikisha wanadamu wachache waaminifu watawale pamoja na Yesu Kristo katika Ufalme wa mbinguni
Luka 12:32: “Msiogope, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.”
Ufu. 14:1-3: “Nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000 . . . ambao wamenunuliwa kutoka duniani.” (Ona ukurasa wa 202, 203, chini ya kichwa, “Mbingu.”)
Wanadamu hawawezi kwenda mbinguni wakiwa na miili ya nyama na damu
1 Kor. 15:50: “Hili nasema, akina ndugu, kwamba nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala uharibifu haurithi kutoweza kuharibika.”
Yoh. 3:6: “Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho.”
Ni wale tu ambao ‘wamezaliwa mara ya pili,’ na kuwa wana wa Mungu, ndio wanaoweza kutawala katika Ufalme wa mbinguni
Yoh. 1:12, 13: “Wengi kadiri ileile waliompokea [Yesu Kristo], aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu, kwa sababu walikuwa wakionyesha imani katika jina lake; nao walizaliwa, si kutokana na damu au kutokana na mapenzi ya mwili au kutokana na mapenzi ya mwanadamu, bali kutokana na Mungu.” (Maneno “wengi kadiri ileile waliompokea” hayamaanishi wanadamu wote ambao wamemwamini Kristo. Ona ni nani wanaorejezewa, kama inavyoonyeshwa katika mstari wa 11 [“watu wake mwenyewe,” Wayahudi]. Wanadamu wengine pia wamepata pendeleo hilohilo, lakini ni “kundi dogo” tu.)
Rom. 8:16, 17: “Roho yenyewe hutoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Basi, ikiwa sisi ni watoto, sisi pia ni warithi: warithi wa Mungu kwelikweli, lakini warithi pamoja na Kristo, mradi tu tunateseka pamoja ili pia tutukuzwe pamoja.”
1 Pet. 1:3, 4: “Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwa maana kulingana na rehema yake kubwa alituzaa sisi upya kwenye tumaini lililo hai kupitia ufufuo wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu, kwenye urithi usioharibika na usiotiwa unajisi na usiofifia. Huo umewekwa akiba mbinguni kwa ajili yenu.”
Watafanya nini mbinguni?
Ufu. 20:6: “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.”
1 Kor. 6:2: “Je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu?”
Je, mtu ambaye ‘hajazaliwa mara ya pili’ anaweza kuokolewa?
Ufu. 7:9, 10, 17: “Baada ya mambo haya [baada ya mtume Yohana kusikia hesabu ya wale ambao ‘wangezaliwa mara ya pili,’ wale ambao wangefanyiza Israeli wa kiroho na ambao wangekuwa pamoja na Kristo mbinguni; linganisha na Waroma 2:28, 29 na Wagalatia 3:26-29] nikaona, na, tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha, wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa kanzu nyeupe; na kulikuwa na matawi ya mitende mikononi mwao. Nao wanaendelea kupaaza sauti kubwa, wakisema: ‘Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi juu ya kiti cha ufalme, na Mwana-Kondoo.’ . . .
-