-
“Ninavipenda Vikumbusho Vyako”Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
-
-
14, 15. (a) Kwa nini tunapendezwa na simulizi la Yosefu? (b) Kwa nini mwanamke mmoja Mkristo anafurahi kwamba alifuata vikumbusho vya Mungu?
14 Yosefu alilelewa katika familia inayomwogopa Mungu, naye alijua kwamba ni kosa kwa watu ambao si mume na mke kufanya ngono pamoja. Aliuliza hivi: “Ninawezaje kufanya ubaya huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?” Huenda alikata kauli hiyo kwa sababu alijua ile kanuni ambayo Mungu aliwapa wanadamu huko Edeni, yaani, kanuni ya kuwa na mume mmoja na mke mmoja. (Mwanzo 2:24)
-