Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dhambi ya Kwanza Ilikuwa Nini?
    Amkeni!—2006 | Juni
    • Walikatazwa tu mti mmoja, yaani, “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” Kwa kuwa walikuwa na uhuru wa kuchagua, Adamu na Hawa wangeweza kuchagua kumtii Mungu au kutomtii. Hata hivyo, Adamu alikuwa ameonywa hivi: “Siku utakapokula [kutokana na mti wa ujuzi], utakufa hakika.”—Mwanzo 1:29; 2:17.

      Kizuizi Kinachofaa

      Kizuizi hicho kimoja hakikutokeza ugumu wowote; Adamu na Hawa wangeweza kula matunda ya miti mingine yote ya bustani. (Mwanzo 2:16) Isitoshe, katazo hilo halikudokeza kwamba wanadamu hao walikuwa na maelekeo ya kutenda mabaya, wala halikuwapokonya adhama yao. Ikiwa Mungu angekuwa amewakataza mambo maovu kama vile kufanya ngono na wanyama au kuua, wengine wangeweza kudai kwamba wanadamu wakamilifu walikuwa na maelekeo fulani mabaya ambayo wangepaswa kuyazuia. Hata hivyo, kula kulikuwa jambo la kawaida na linalofaa.

      Je, tunda lililokatazwa lilikuwa ngono kama watu fulani wanavyoamini? Biblia haiungi mkono maoni hayo. Jambo moja linalopaswa kuzingatiwa ni kwamba Mungu alipoweka katazo hilo, Adamu alikuwa peke yake na yaonekana aliendelea kuwa peke yake kwa muda fulani. (Mwanzo 2:23) Pili, Mungu aliwaambia Adamu na Hawa ‘wazae, wawe wengi na kuijaza dunia.’ (Mwanzo 1:28) Bila shaka, hangewaamuru wavunje amri yake kisha awahukumu kifo kwa kufanya hivyo! (1 Yohana 4:8) Tatu, Hawa alikula tunda hilo kabla ya Adamu kisha baadaye akampa mumewe. (Mwanzo 3:6) Ni wazi kwamba tunda hilo halikuwa ngono.

      Wajaribu Kujiamulia Mema na Mabaya

      Mti wa ujuzi ulikuwa mti halisi. Hata hivyo, uliwakilisha haki ya Mungu akiwa Mtawala ya kuamulia wanadamu mema na mabaya. Kwa hiyo, kula matunda ya mti huo hakukuwa tu wizi, yaani, kuchukua kitu kilichokuwa mali ya Mungu, bali pia kulikuwa jitihada ya kujiamulia mema na mabaya. Ona kwamba baada ya kumdanganya Hawa kwamba iwapo yeye na mume wake wangekula tunda hilo, ‘hawangekufa hakika,’ Shetani alisisitiza hivi: “Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”—Mwanzo 3:4, 5.

  • Dhambi ya Kwanza Ilikuwa Nini?
    Amkeni!—2006 | Juni
    • Ni kweli kwamba waliishi kwa mamia ya miaka, lakini walianza kufa “siku” ambayo walitenda dhambi, sawa na vile tawi huanza kufa linapokatwa kutoka kwenye mti. (Mwanzo 5:5)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki