-
Kwa Nini Uovu UnaendeleaMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
Hawa aliporudia kutaja amri ya Mungu, Shetani akamwambia hivi: “Hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
-
-
Kwa Nini Uovu UnaendeleaMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
Je, unaona uzito wa yale yaliyotukia? Ibilisi alipinga yale ambayo Mungu alikuwa amemwambia Adamu. Maneno ya Shetani yalimaanisha kwamba Adamu na Hawa hawangemhitaji Yehova awaamulie yaliyo mema na yaliyo mabaya. Kwa hiyo, suala ambalo Shetani alitokeza lilitilia shaka haki na uhalali wa utawala wa Yehova juu ya mwanadamu. Basi, suala muhimu sana ambalo Shetani alitokeza lilihusu haki ya Yehova ya kuwa mwenye enzi kuu.
-
-
Kwa Nini Uovu UnaendeleaMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
Shetani alimwambia Hawa kwa ujasiri hivi: “Hakika hamtakufa.” (Mwanzo 3:4) Kwa kusema kwamba Adamu na Hawa hawangekufa ikiwa wangekula tunda lililokatazwa, kwa kweli, Shetani alikuwa akimwita Yehova mwongo. Hilo ni shtaka zito sana! Ikiwa Mungu hakusema kweli katika jambo hilo, angeweza jinsi gani kuaminiwa katika jambo lingine lolote? Hata hivyo, wakati umeonyesha nini?
Adamu na Hawa walipata magonjwa, maumivu, walizeeka, na mwishowe wakafa. Biblia inasema hivi: “Siku zote ambazo Adamu aliishi zikajumlika kuwa miaka 930, naye akafa.” (Mwanzo 3:19; 5:5) Wanadamu wote wamerithi matokeo hayo yenye kuhuzunisha kutoka kwa Adamu. (Waroma 5:12) Kupita kwa wakati kumethibitisha kwamba Shetani ni “mwongo na ndiye baba ya uwongo” na kumeonyesha kwamba Yehova ni “Mungu wa ukweli.”—Yohana 8:44; Zaburi 31:5.
-