-
Je, Ni Kosa Kutamka Jina la Mungu?Amkeni!—1999 | Machi 8
-
-
KWA karne nyingi Dini ya Kiyahudi imefunza kwamba jina la Mungu, Yehova, ni takatifu sana kutamkwa.a (Zaburi 83:18) Wanatheolojia wengi wamesababu kwamba ni utovu wa heshima kumwita Muumba mwenye utukufu kwa njia hiyo ya kawaida na hata kwamba kufanya hivyo kunavunja amri ya tatu kati ya zile Amri Kumi, inayokataza ‘kulitaja bure jina la Bwana.’ (Kutoka 20:7) Katika karne ya tatu W.K., Mishnah ilitangaza kwamba “yule anayelitamka Jina la Mungu kama ambavyo limeandikwa” ni mtu ambaye “hana urithi katika ulimwengu ujao.”—Sanhedrini 10:1.
-
-
Je, Ni Kosa Kutamka Jina la Mungu?Amkeni!—1999 | Machi 8
-
-
Ile Amri ya Tatu
Namna gani lile katazo linalotajwa katika Amri ya tatu kati ya zile Amri Kumi? Andiko la Kutoka 20:7 lasisitiza hivi: “Usilitaje bure jina la BWANA [“Yehova,” NW], Mungu wako, maana BWANA [“Yehova,” NW] hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.”
Kulitaja jina la Mungu “bure” kwamaanisha nini hasa? Kitabu The JPS Torah Commentary, kilichochapishwa na Jewish Publication Society, chaeleza kwamba neno la Kiebrania linalotafsiriwa kuwa “bure”(lash·shaw’ʹ) laweza kumaanisha “kwa uongo” au “bila sababu.” Kichapo hicho chaendelea kusema: “Maana nyingi ya [neno hilo la Kiebrania] yatia ndani kuzuia kutekelezwa kwa haki na wahusika wakuu katika mashtaka, kuapa kwa uongo, na kutumia Jina la Mungu isivyo lazima au isivyofaa.”
Ufafanuzi huo wa Kiyahudi wakazia kwa usahihi kwamba ‘kulitaja jina la Mungu bure’ kwahusisha kulitumia jina hilo katika njia isiyofaa. Lakini je, kulitamka jina la Mungu unapowafundisha wengine juu yake au unapomfikia Baba yetu wa kimbingu katika sala kwaweza kwa haki kutajwa kuwa kulitumia jina hilo “isivyo lazima au isivyofaa”? Yehova hueleza maoni yake kwa maneno ya Zaburi 91:14: “Kwa kuwa amekaza kunipenda, nitamwokoa; na kumweka palipo juu, kwa kuwa amenijua Jina langu.”
-