Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”
    Mkaribie Yehova
    • 10 Fikiria mambo yaliyotukia siku za Yeftha. Waisraeli walipoanza kuitumikia miungu ya uwongo, Yehova aliwaacha wateswe na Waamoni kwa miaka 18. Mwishowe, walitubu. Biblia inatuambia hivi: “Nao wakaiondoa hiyo miungu ya kigeni iliyokuwa kati yao, nao wakamtumikia BWANA; na roho yake ilihuzunika kwa sababu ya msiba wa Israeli.”b (Waamuzi 10:6-16) Mara tu baada ya watu wake kutubu kikweli, Yehova hakuweza kuvumilia kuwaona wakiteseka. Kwa hiyo, Mungu mwenye huruma nyororo alimpa Yeftha nguvu ili awakomboe Waisraeli kutoka mikononi mwa adui zao.—Waamuzi 11:30-33.

  • “Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”
    Mkaribie Yehova
    • b Usemi unaotafsiriwa “roho yake ilihuzunika” wamaanisha kihalisi ‘subira yake ilifikia kikomo.’ Biblia Habari Njema yasema: “Hakuweza kuvumilia zaidi kuona taabu za Waisraeli.” Kichapo Tanakh—A New Translation of the Holy Scriptures chasema hivi: “Hakuweza kustahimili kuona Israeli ikitaabika.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki