Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mwanamke Bora Sana”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Oktoba 1
    • Akichochewa na jambo hilo, Naomi akajibu: “Na abarikiwe huyo na Yehova, ambaye hakuacha kuonyesha fadhili zake zenye upendo kwa walio hai na wafu.” (Ruthu 2: 19, 20) Aliona fadhili za Boazi kuwa zinatoka kwa Yehova, ambaye anachochea watumishi wake wawe wakarimu na ambaye ameahidi kuwathawabisha watu wake kwa sababu ya fadhili wanazoonyesha.b​—Methali 19:17.

  • “Mwanamke Bora Sana”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Oktoba 1
    • Ruthu alipomtaja Boazi kwa mara ya kwanza, Naomi alisema: “Mwanamume huyo ni wa jamaa yetu. Yeye ni mmoja wa wakombozi wetu.” (Ruthu 2: 20) Alimaanisha nini? Sheria ya Mungu kwa Waisraeli ilikuwa na mpango wenye upendo kwa familia ambazo ziliteseka kwa sababu ya umaskini au kufiwa. Ikiwa mwanamke angekuwa mjane asiye na mtoto, alikatishwa tamaa kwa sababu jina la mume wake, yaani, uzao wake, haungejulikana na vizazi vya wakati ujao. Hata hivyo, Sheria ya Mungu ilimruhusu ndugu ya mwanamume huyo amwoe yule mjane ili amzalie mrithi ambaye angeendeleza jina la mume aliyekufa na kutunza mali ya familia.c​—Kumbukumbu la Torati 25:5-7.

  • “Mwanamke Bora Sana”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Oktoba 1
    • b Kama Naomi alivyosema, Yehova hawaonyeshi tu fadhili walio hai; bali pia watu waliokufa. Naomi alikuwa amefiwa na mumewe na wanawe wawili. Naye Ruthu alikuwa amefiwa na mumewe. Bila shaka, wanaume hao watatu walipendwa sana na wanawake hawa wawili. Fadhili zozote ambazo Ruthu na Naomi walionyeshwa, zilikuwa fadhili kuelekea wanaume hao ambao pia wangetaka wanawake hawa wapendwa watunzwe.

      c Inaelekea kwamba ndugu ya mwanamume aliyekufa ndiye aliyepewa kwanza haki ya kuoa mjane kama huyo kisha mtu wa ukoo wa karibu zaidi, kama vile haki ya kupokea urithi ilivyokuwa.—Hesabu 27:5-11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki