Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alimmwagia Mungu Mahangaiko Yake Kupitia Sala
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Julai 1
    • Hana alipommiminia Yehova moyo wake na kumwabudu katika maskani, kulikuwa na matokeo gani? Simulizi hilo linasema: “Mwanamke huyo akaenda zake, akala chakula, na uso wake haukuonyesha tena kuhangaika.” (1 Samweli 1:18) Biblia Habari Njema inasema: “Hakuwa na huzuni tena.” Hana alihisi ametulia. Ni kana kwamba alikuwa amechukua mzigo wake wa hisia zilizokuwa zikimfadhaisha na kumtupia Yehova, Baba yake wa mbinguni mwenye nguvu. (Zaburi 55:22) Je, Yehova anaweza kushindwa na tatizo lolote? La—hakuna lolote lililomshinda jana, linaloweza kumshinda leo, wala kesho!

      Tunapohisi tumelemewa na hisia au kuhuzunika kupita kiasi, tunaweza kumwiga Hana na kuzungumza waziwazi na Yule ambaye Biblia inamwita “msikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Tukisali kwa imani, huenda tukaacha kuhuzunika na badala yake tukawa na “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”—Wafilipi 4:6, 7.

  • Alimmwagia Mungu Mahangaiko Yake Kupitia Sala
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Julai 1
    • Ni wakati gani ambapo Penina alitambua kuwa hangeweza tena kumhuzunisha Hana? Simulizi halitaji hilo, lakini maneno uso wa Hana “haukuonyesha tena kuhangaika” yanaonyesha kwamba kuanzia wakati huo Hana alidumisha furaha yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki