-
Ziara Iliyothawabishwa SanaMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 1
-
-
Walifanya Mapenzi ya Yehova
Ziara Iliyothawabishwa Sana
LAZIMA malkia awe alichoshwa sana na safari ya kutoka Sheba hadi Yerusalemu. Alikuwa amezoea kuishi maisha ya anasa. Sasa alikuwa akisafiri kwa mwendo wa ngamia safari iliyokuwa na urefu wa kilometa 2,400, sehemu kubwa ikiwa katika jangwa lenye joto jingi. Kulingana na kadirio moja, huenda safari yake, ya kwenda tu hadi huko, ilichukua siku zipatazo 75 kuikamilisha!a
Ni kwa nini malkia huyo mwenye mali nyingi aliacha makao yake yenye starehe katika Sheba na kufunga safari ngumu hivyo?
Ripoti Yenye Kuvutia
Malkia wa Sheba alikuja Yerusalemu baada ya “[ku]sikia habari za Sulemani juu ya jina la BWANA.” (1 Wafalme 10:1) Habari kamili ambayo malkia alisikia haijaelezwa. Hata hivyo, twajua kwamba Yehova alimpa Solomoni baraka ya hekima, mali, na heshima kwa njia ya pekee. (2 Mambo ya Nyakati 1:11, 12) Malkia alikuja kujuaje hayo? Kwa kuwa Sheba ilikuwa kitovu cha biashara, huenda alisikia juu ya umaarufu wa Solomoni kupitia wafanyabiashara waliozuru nchi yake. Labda baadhi ya watu hao walikuwa wamezuru Ofiri, nchi ambayo Solomoni alifanya nayo biashara nyingi.—1 Wafalme 9:26-28.
-
-
Ziara Iliyothawabishwa SanaMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 1
-
-
Hata hivyo, ona kwamba malkia alisikia umaarufu wa Solomoni “juu ya jina la BWANA.” Hivyo, safari hiyo haikuwa ya kibiashara tu. Yamkini, malkia alikuja hasa kusikiliza hekima ya Solomoni—labda hata kujifunza jambo fulani kuhusu Mungu wa Solomoni, Yehova. Kwa vile yawezekana alikuwa wa uzao wa Shemu ama Hamu, waliokuwa waabudu wa Yehova, huenda alikuwa mdadisi kuhusu dini ya mababu wake.
Maswali ya Fumbo, Majibu Yenye Kuridhisha
Alipokutana na Solomoni, malkia akaanza kumjaribu kwa “maswali ya fumbo.” (1 Wafalme 10:1) Neno la Kiebrania lililotumiwa hapo laweza kutafsiriwa “vitendawili.” Lakini hilo halimaanishi kwamba malkia alimwingiza Solomoni katika michezo isiyo na maana. Kwa kupendeza, katika Zaburi 49:4 (BHN), neno hilohilo la Kiebrania limetumiwa kufafanua maswali mazito yanayohusu dhambi, kifo, na ukombozi. Basi, yaonekana kuwa malkia wa Sheba alikuwa akizungumza na Solomoni habari nzito zilizojaribu kina cha hekima yake.
-