Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Kuna Thawabu kwa Ajili ya Kazi Yenu”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 15
    • Iweni hodari na msiache mikono yenu ilegee, kwa sababu kuna thawabu kwa ajili ya kazi yenu.”​—2 Nya. 15:1, 2, 7.

  • “Kuna Thawabu kwa Ajili ya Kazi Yenu”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 15
    • Azaria alisema hivi: “Iweni hodari.” Kwa kawaida, uhodari mkubwa unahitajiwa ili kufanya mambo yanayofaa, lakini tunajua kwamba tunaweza kufanikiwa kwa msaada wa Yehova.

      Kwa kuwa Maaka, nyanya ya Asa alitengeneza “sanamu yenye kutisha kwa ajili ya mti mtakatifu,” Asa alikuwa na kazi ngumu ya kumwondoa ili asiendelee kuwa “malkia.” Alishinda jaribu hilo na kuteketeza sanamu iliyotengenezwa na nyanya yake. (1 Fal. 15:13) Asa alibarikiwa kwa sababu ya azimio na uhodari wake. Sisi pia ni lazima tushikamane kabisa na Yehova na viwango vyake vya uadilifu iwe watu wetu wa ukoo ni washikamanifu kwa Mungu au la. Tukifanya hivyo, Yehova atatuthawabisha kwa sababu ya mwenendo wetu wa uaminifu.

      Asa alithawabishwa alipowaona Waisraeli wengi kutoka katika ufalme wa kaskazini wenye kuasi imani wakimiminika Yuda walipoona kwamba Yehova alikuwa pamoja naye. Walithamini sana ibada safi hivi kwamba wakaamua kuacha nyumba zao ili waishi miongoni mwa watumishi wa Yehova. Kisha, Asa na watu wote katika Yuda wakafurahi na ‘kuingia katika agano ili kumtafuta Yehova Mungu kwa moyo wao wote na kwa nafsi yao yote.’ Ikawaje? Mungu “aliwaruhusu wampate; na Yehova akaendelea kuwapa pumziko kuzunguka pande zote.” (2 Nya. 15:9-15)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki