-
Yehova na Apendezwe na Hesabu YakoMnara wa Mlinzi—1996 | Septemba 15
-
-
2. (a) Nehemia alitoa hesabu njema kwa Mungu kujihusu mwenyewe katika njia zipi? (b) Nehemia alimalizia kitabu cha Biblia chenye jina lake kwa ombi jipi?
2 Mtu mmoja aliyetoa hesabu njema kwa Mungu kujihusu mwenyewe, alikuwa Nehemia, mnyweshaji wa Mfalme wa Uajemi Artashasta (Longimano). (Nehemia 2:1) Nehemia alipata kuwa gavana wa Wayahudi, akajenga upya ukuta wa Yerusalemu akikabili maadui na hatari mbalimbali. Akiwa na bidii kwa ajili ya ibada ya kweli, alitekeleza Sheria ya Mungu na kuwaonyesha ufikirio wale walioonewa. (Nehemia 5:14-19) Nehemia aliwasihi sana Walawi wajisafishe kwa ukawaida, walinde malango, na kutakasa siku ya Sabato. Kwa hiyo aliweza kusali hivi: “Hili, nalo, ulikumbuke kwenye hesabu yangu, Ee Mungu wangu, na unisikitikie kulingana na wingi wa fadhili-upendo zako.” Pia, kwa kufaa, Nehemia alimalizia hivi, kitabu chake kilichopuliziwa kimungu: “Unikumbuke, Ee Mungu wangu, kwa ajili ya mema.”—Nehemia 13:22, 31, NW.
-
-
Yehova na Apendezwe na Hesabu YakoMnara wa Mlinzi—1996 | Septemba 15
-
-
“Hili . . . ulikumbuke kwenye hesabu yangu, Ee Mungu wangu . . . Unikumbuke, Ee Mungu wangu, kwa ajili ya mema.”—NEHEMIA 13:22, 31, NW.
-