-
Ayubu Alilitukuza Jina la YehovaMnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
-
-
6. (a) Ni jambo gani lililotukia katika mkutano mwingine huko mbinguni? (b) Shetani alikuwa akimfikiria nani alipotilia shaka utimilifu wa Ayubu kwa Yehova?
6 Baadaye, kulikuwa na mkutano mwingine mbinguni. Kwa mara nyingine tena Shetani alimshtaki Ayubu, akisema: “Ngozi kwa ngozi, na kila kitu alicho nacho mtu atakitoa kwa ajili ya nafsi yake. Ili kuwe na badiliko, tafadhali nyoosha mkono wako, uguse kufikia mfupa wake na nyama yake, uone kama hatakulaani wewe mbele za uso wako.” Ona kwamba Shetani alihusisha watu wengine katika mashtaka yake. Kwa kusema, “Kila kitu alicho nacho mtu atakitoa kwa ajili ya nafsi yake,” Ibilisi hakutilia shaka utimilifu wa Ayubu tu, bali pia wa “mtu” yeyote yule anayemwabudu Yehova.
-