-
Ninaweza Kuwa Rafiki ya Mungu Jinsi Gani?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
Mtunga-zaburi Daudi aliandika: “Onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema.” (Zaburi 34:8) Daudi alitunga Zaburi ya 34 baada ya kupitia hali yenye kuogopesha. Alikuwa akimkimbia Mfalme Sauli aliyetaka kumwua—masaibu kwelikweli. Kisha akalazimika kutafuta kimbilio kati ya Wafilisti waliokuwa maadui. Uhai wake ulipokuwa hatarini, Daudi alijifanya mwenda-wazimu na kukimbia.—1 Samweli 21:10-15.
Daudi hakuona kwamba alikuwa ameponea chupuchupu kwa sababu ya werevu wake mwenyewe. Badala yake, alisema kwamba wokovu wake ulitokana na Yehova. Mapema katika zaburi iliyotajwa, aliandika: “Nilimuuliza Yehova, naye akanijibu, naye akanikomboa kutoka katika mambo yote yenye kuniogopesha.” (Zaburi 34:4) Mambo aliyojionea mwenyewe yalimchochea Daudi kuwahimiza wengine ‘waonje na kuona ya kuwa Yehova ni mwema.’a
-
-
Ninaweza Kuwa Rafiki ya Mungu Jinsi Gani?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
a Biblia nyingine hutafsiri maneno “onjeni mwone,” kuwa “jigundulie mwenyewe,” “jionee mwenyewe,” na “kupitia mambo utakayojionea utaona kwamba.”—Contemporary English Version, Today’s English Version, na The Bible in Basic English.
-