-
Yehova Hutujulisha Jinsi ya Kuzihesabu Siku ZetuMnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 15
-
-
Yehova—“Makao Halisi” Kwetu
4-6. Yehova ni “makao halisi” kwetu jinsi gani?
4 Mtunga-zaburi anaanza kwa kusema: “Ee Yehova, wewe mwenyewe umekuwa makao halisi kwetu, kizazi baada ya kizazi.
-
-
Yehova Hutujulisha Jinsi ya Kuzihesabu Siku ZetuMnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 15
-
-
5 Yehova, “Mungu adumuye milele,” amekuwa “makao halisi” kwetu—kimbilio la kiroho. (Waroma 16:26) Tunahisi tukiwa salama kwa kuwa yeye yu tayari sikuzote kutusaidia akiwa “Msikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2, NW) ‘Amani ya Mungu izidiyo fikira yote kwa ubora hulinda mioyo yetu na nguvu zetu za akili’ kwa kuwa sisi humtwika Baba yetu wa mbinguni mahangaiko yetu kupitia Mwanaye mpendwa.—Wafilipi 4:6, 7; Mathayo 6:9; Yohana 14:6, 14.
6 Tunafurahia usalama wa kiroho kwa sababu, kwa njia ya mfano, Yehova ni “makao halisi” kwetu. Yeye pia huandaa “vyumba”—ambavyo yaelekea vyahusiana sana na makutaniko ya watu wake. “Vyumba” hivyo ni kimbilio la kiroho, ambapo wachungaji wenye upendo hutusaidia sana kuhisi tukiwa salama. (Isaya 26:20; 32:1, 2; Matendo 20:28, 29) Isitoshe, baadhi yetu tumetoka katika familia za watu ambao wamemtumikia Mungu kwa muda mrefu na wametambua kwamba yeye ni ‘makao halisi kizazi baada ya kizazi.’
-