-
Yehova Hutujulisha Jinsi ya Kuzihesabu Siku ZetuMnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 15
-
-
Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie moyo wa hekima.” (Zaburi 90:11, 12)
-
-
Yehova Hutujulisha Jinsi ya Kuzihesabu Siku ZetuMnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 15
-
-
19 Maneno ya mtunga-zaburi ni sala kwa Yehova kwamba awafundishe watu wake jinsi ya kutumia hekima katika kuzihesabu na kuzitumia siku zinazobaki za maisha yao kwa njia inayokubaliwa na Mungu. Mtu anayetarajia kuishi miaka 70 ana tumaini la kuishi siku 25,500 hivi. Lakini, hata tuwe na umri gani, ‘hatujui uhai wetu utakuwa nini kesho, kwa maana sisi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka.’ (Yakobo 4:13-15) Kwa kuwa ‘wakati na tukio lisilotazamiwa hutupata sote,’ hatujui tutaishi kwa muda mrefu kadiri gani. Kwa hiyo, na tusali tuwe na hekima ya kukabiliana na majaribu, kuwatendea wengine ifaavyo, na kufanya yote tunayoweza katika utumishi wa Yehova sasa—leo! (Mhubiri 9:11; Yakobo 1:5-8) Yehova hutuongoza kupitia Neno lake, roho yake, na tengenezo lake. (Mathayo 24:45-47; 1 Wakorintho 2:10; 2 Timotheo 3:16, 17) Kutumia hekima hutuchochea ‘tutafute kwanza Ufalme wa Mungu’ na kuzitumia siku zetu katika njia inayomtukuza Yehova na kuufurahisha moyo wake. (Mathayo 6:25-33; Mithali 27:11) Bila shaka, kumwabudu kwa moyo wote hakutatuondolea matatizo yetu yote, lakini tuna hakika kwamba kufanya hivyo kutaleta baraka nyingi.
-