Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Aliyetunga Sheria Zinazoongoza Ulimwengu Wetu?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 1
    • 3. Je, Ulimwengu Unadumu Milele au Unaweza Kuharibika?

      Aristoto aliamini kwamba kuna tofauti kubwa kati ya mbingu zenye nyota na dunia. Alisema kwamba dunia inaweza kubadilika, kuharibika, na kuchakaa, lakini mbingu zenye nyota haziwezi kubadilika, zinadumu milele. Aliamini kuwa miviringo aliyotaja na nyota ambazo zimeshikizwa kwenye miviringo hiyo haziwezi kubadilika, kuchakaa, wala kutoweka.

      Je, Biblia inafundisha hivyo? Andiko la Zaburi 102:25-27 linasema: “Wewe uliiweka misingi ya dunia zamani za kale, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako. Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama; nazo zote zitachakaa kama vazi. Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake. Lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako mwenyewe haitamalizika.”

      Ona kwamba mtunga-zaburi huyo aliyeandika maneno hayo yapata miaka 200 kabla ya siku za Aristoto, hasemi kuna tofauti kati ya dunia na mbingu zenye nyota, kana kwamba dunia inaweza kuharibika na nyota kudumu milele. Badala yake, anaonyesha kwamba mbingu na dunia ni tofauti kabisa na Yehova Mungu. Hivyo, Yehova ambaye ni Roho mwenye nguvu ndiye aliyeelekeza mbingu na dunia ziumbwe.d Zaburi hii inaonyesha kwamba nyota zinaweza kuharibika sawa na vitu vingine duniani. Lakini wanasayansi wa kisasa wamevumbua nini?

      Wanajiolojia (wataalamu wa miamba ya dunia) wanaunga mkono maoni ya Biblia na ya Aristoto kwamba dunia inaweza kuharibika. Bila shaka, mawe ya dunia yetu yanaendelea kumomonyoka na mengine kutokea kupitia milipuko ya volkano na mabadiliko mengine yanayotokea katika miamba iliyo chini ya ardhi.

      Namna gani nyota? Je, zinaweza kuharibika, kama Biblia inavyodokeza, au zinadumu milele, kama Aristoto alivyofundisha? Katika karne ya 16 W.K., wataalamu wa nyota barani Ulaya walianza kutilia shaka maoni ya Aristoto kwamba nyota zinadumu milele wakati ambapo, kwa mara ya kwanza, waliona nyota ikilipuka. Tangu wakati huo wanasayansi wametambua kwamba nyota zinaweza kulipuka kwa nguvu na kutoweka au kuteketea polepole, au hata kuzimika. Lakini, wataalamu wa nyota wameona nyota mpya zikitokea kwenye mawingu ya gesi ambayo yanafanywa kuwa mazito na vumbi linalotokana na nyota zilizolipuka. Hivyo, mfano wa mwandikaji wa Biblia kuhusu vazi linalochakaa na kubadilishwa unafaa kabisa.e Ni jambo la ajabu kama nini kwamba mtunga-zaburi huyo wa kale aliandika maneno yanayopatana vizuri na uvumbuzi wa siku hizi!

      Hata hivyo, huenda ukauliza: ‘Je, Biblia inafundisha kwamba wakati fulani dunia au mbingu zenye nyota zitafikia kikomo au zihitaji kubadilishwa?’ Hapana, Biblia inaahidi kwamba zitadumu milele. (Zaburi 104:5; 119:90) Lakini hilo halimaanishi kwamba vitu hivyo ni vya milele; badala yake, Mungu aliyeviumba ameahidi kuvidumisha. (Zaburi 148:4-6) Hasemi jinsi atakavyofanya hivyo, lakini ni jambo linalopatana na akili kusema kwamba Muumba wa ulimwengu ana uwezo wa kuudumisha, sawa na vile mjenzi stadi anavyoweza kuitunza vizuri nyumba aliyojenga kwa ajili yake mwenyewe na familia yake.

  • Ni Nani Aliyetunga Sheria Zinazoongoza Ulimwengu Wetu?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 1
    • e Katika karne ya 19, mwanasayansi William Thomson, ambaye pia anaitwa Lord Kelvin, alivumbua sheria ya pili kuhusu uhusiano kati ya joto na aina nyingine za nishati, inayoeleza kwa nini baada ya muda, mfumo wa asili huanza kuharibika na kubadilika. Alielewa sheria hiyo baada ya kuchunguza kwa makini Zaburi 102: 25-27.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki