-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
Kutumia Utajiri kwa Hekima
9, 10. Wakristo wa kweli wametumia jinsi gani utajiri wao wa kiroho, na uadilifu wao utasimama milele jinsi gani?
9 “Vitu vyenye thamani na utajiri vimo nyumbani mwake; nao uadilifu wake unasimama milele. Ameangaza katika giza kama nuru kwa walio wanyoofu. Yeye ni mwenye neema na mwenye rehema na mwadilifu.” (Zab. 112:3, 4) Katika nyakati za Biblia, watumishi fulani wa Mungu walijulikana kwa sababu ya utajiri wao. Na katika maana nyingine, wale ambao wana kibali cha Mungu wanakuwa matajiri kikweli, hata ikiwa si kimwili. Ukweli ni kwamba, wale ambao wanaamua kujinyenyekeza machoni pa Mungu huenda wakawa maskini na wenye kudharauliwa, kama ilivyokuwa katika siku za Yesu. (Luka 4:18; 7:22; Yoh. 7:49) Lakini iwe mtu ana vitu vingi au vichache vya kimwili, anaweza kuwa tajiri kiroho.—Mt. 6:20; 1 Tim. 6:18, 19; soma Yakobo 2:5.
-
-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
Wapinzani wamejaribu kusimamisha kazi ya kuhubiri Ufalme lakini wameshindwa. Badala yake, matunda ya kazi hiyo ya uadilifu ‘yatasimama milele.’ Kwa kubaki waadilifu chini ya majaribu, watumishi wa Mungu wanaweza kuwa na uhakika wa kuishi daima, ‘kusimama milele.’
-