-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
11, 12. Watu wa Mungu wanatumia vitu vyao vya kimwili katika njia gani?
11 Watu wa Mungu, wale wa jamii ya mtumwa ambaye ni mtiwa-mafuta na wale wa “umati mkubwa,” wamejithibitisha kuwa wakarimu kuhusiana na vitu vya kimwili. Zaburi 112:9 inasema hivi: “Amegawa kwa wingi; amewapa maskini.” Mara nyingi, Wakristo wa kweli leo wanatoa michango kwa ajili ya Wakristo wenzao na hata kwa ajili ya majirani wao wenye uhitaji. Pia, wanatumia mali za kimwili ili kutegemeza kampeni za kutoa misaada wakati wa misiba. Kama Yesu alivyoonyesha, furaha ya kweli inatokana pia na kutoa.—Soma Matendo 20:35; 2 Wakorintho 9:7.
12 Zaidi ya hayo, fikiria gharama za kuchapisha gazeti hili katika lugha 172, na nyingi ya lugha hizo zinazungumzwa na watu ambao ni maskini. Fikiria pia ukweli wa kwamba gazeti hili linapatikana katika lugha mbalimbali za ishara zinazotumiwa na viziwi, na pia katika maandishi ya vipofu.
-
-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
‘Kuinuliwa kwa Utukufu’
17. Mwadilifu ‘atainuliwa kwa utukufu’ jinsi gani?
17 Itakuwa shangwe kama nini kumsifu Yehova kwa umoja, bila upinzani kutoka kwa Ibilisi na ulimwengu wake! Wote ambao wanadumisha msimamo wa uadilifu machoni pa Mungu watamsifu kwa furaha milele. Hawatashindwa, kwa kuwa Yehova anaahidi pia kwamba “pembe” ya mwadilifu “itainuliwa kwa utukufu.” (Zab. 112:9) Mwadilifu wa Yehova atashangilia kwa ushindi atakapoona maadui wote wa enzi kuu ya Yehova wakishindwa.
-