-
Wote na Wautangaze Utukufu wa YehovaMnara wa Mlinzi—2004 | Januari 1
-
-
Kamba yake ya kupimia imefika duniani pote, na maneno yake yamefika kwenye miisho ya nchi yenye kuzaa.”—Zaburi 19:1, 4.
2 Mbingu zenye kutia woga ambazo Yehova aliumba hutangaza utukufu wake siku baada ya siku, usiku baada ya usiku, bila usemi, maneno, wala sauti. Uumbaji haukomi kamwe kuutangaza utukufu wa Mungu, na hilo hutunyenyekeza tutafakari ushuhuda huo wa kimya-kimya ambao huonekana “duniani pote” na wakaaji wote wa dunia. Hata hivyo, ushahidi ambao uumbaji unatoa kimya-kimya hautoshi.
-
-
Wote na Wautangaze Utukufu wa YehovaMnara wa Mlinzi—2004 | Januari 1
-
-
Paulo anaonyesha jambo hilo kwa kunukuu andiko la Zaburi 19:4 na kuonyesha kwamba linahusiana na kazi ya Kikristo ya kuhubiri wala si ule ushahidi wa kimya-kimya unaotolewa na uumbaji. Anasema hivi: “Kwani, kwa kweli, ‘sauti yao ilifika katika dunia yote, na maneno yao mpaka miisho ya dunia inayokaliwa.’” (Waroma 10:16, 18) Naam, kama vile uumbaji usio na uhai unavyomtukuza Yehova, Wakristo wa karne ya kwanza walihubiri kila mahali habari njema za wokovu na hivyo kumtukuza Mungu “duniani pote.” Katika barua yake kwa Wakolosai, Paulo pia alieleza jinsi habari njema zilivyokuwa zimehubiriwa kwa mapana na marefu. Alisema kwamba habari njema zilikuwa zimehubiriwa “katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu.”—Wakolosai 1:23.
-