-
“Uzishike Amri Zangu Ukaishi”Mnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 15
-
-
Moyo wako usizielekee njia zake, wala usipotee katika mapito yake.
-
-
“Uzishike Amri Zangu Ukaishi”Mnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 15
-
-
Kwa wazi, Solomoni atushauri tuepuke njia zenye kuleta kifo za mtu asiye na adili na ‘kuendelea kuishi.’ (Mithali 7:2) Shauri hilo linafaa wakati wetu kama nini! Kwa hakika kuna uhitaji wa kuepuka sehemu ambazo hutembelewa mara kwa mara na watu wanaootea ili kunasa wengine. Kwa nini unaswe na mbinu zao kwa kwenda mahali kama hapo? Kwa kweli, kwa nini uwe mmoja wa ‘wasio na akili’ na kutangatanga katika njia za “mgeni”?
“Mgeni” ambaye mfalme aliona alimtongoza kijana kwa kumwalika ‘wajifurahishe nafsi zao kwa mahaba.’ Je, vijana wengi—hasa wasichana—hawajadanganywa kwa njia kama hiyo? Lakini fikiria jambo hili: Mtu fulani anapojaribu kukutongoza ujihusishe na mwenendo usiofaa kingono, je, huo ni upendo halisi au ni uchu wa kibinafsi? Kwa nini mwanamume anayempenda mwanamke kikweli amsonge kukiuka dhamiri yake na mafunzo ya Kikristo aliyopata? ‘Moyo wako usizielekee’ njia hizo, ashauri Solomoni.
-