Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Kwa Hekima Siku Zetu Zitazidishwa’
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Mei 15
    • njoo ule mkate wangu, ukanywe divai niliyoichanganya. Enyi wajinga, acheni ujinga, mkaishi, mkaende katika njia ya ufahamu.”—Mithali 9:3-6.

  • ‘Kwa Hekima Siku Zetu Zitazidishwa’
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Mei 15
    • Nao wanatolewa ahadi ya uhai. Karibu watu wote wanaweza kujipatia hekima ya Neno la Mungu, kutia ndani hekima inayopatikana katika kitabu cha Mithali. Leo, Mashahidi wa Yehova ambao ni wajumbe wa hekima ya kweli, wanajitahidi sana kuwaalika watu kila mahali wajifunze Biblia. Kutwaa ujuzi huo, kunaweza kuongoza kwenye uhai udumuo milele.—Yohana 17:3.

      Wakristo wanapaswa kukubali kwa unyenyekevu nidhamu ambayo hutolewa na hekima. Jambo hilo ni kweli hasa kuhusu vijana na wale ambao wameanza majuzi kujifunza juu ya Yehova. Kwa sababu hawana ujuzi mwingi kuhusu njia za Mungu huenda ‘wasiwe na ufahamu.’ Haimaanishi kwamba makusudio yao yote ni mabaya. Lakini ili nia na makusudio yao ya moyoni yampendeze Yehova Mungu, kutumia wakati na jitihada nyingi huhitajika. Wanahitaji kurekebisha mawazo, tamaa, mapendezi, na miradi yao ili kuzipatanisha na mapenzi ya Mungu. Lazima ‘wafanyize hamu sana ya maziwa yasiyoghushiwa yaliyo ya neno.’—1 Petro 2:2.

      Sisi sote tunapaswa ‘kuacha fundisho la msingi.’ Lazima sisi sote tusitawishe upendezi kwa “mambo yenye kina kirefu ya Mungu” na kupata lishe kutokana na chakula kigumu ambacho ni cha watu wakomavu. (Waebrania 5:12–6:1; 1 Wakorintho 2:10) “Mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” ambaye anaongozwa moja kwa moja na Yesu Kristo, anaandaa kwa bidii chakula cha kiroho cha wakati unaofaa kwa wote. (Mathayo 24:45-47) Acheni tule kwenye meza iliyopangwa na hekima kwa kujifunza kwa bidii Neno la Mungu na vichapo vya Biblia ambavyo vimeandaliwa na jamii ya mtumwa mwaminifu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki