-
Mfanye Yehova Kuwa Tumaini LakoMnara wa Mlinzi—2003 | Septemba 1
-
-
Maana ya Kumtumaini Yehova
18, 19. Biblia inatumia maneno gani kututia moyo tumtumaini Yehova, lakini watu fulani wana maoni gani yasiyofaa kuhusiana na hilo?
18 Neno la Mungu linatuhimiza hivi: “Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
-
-
Mfanye Yehova Kuwa Tumaini LakoMnara wa Mlinzi—2003 | Septemba 1
-
-
Kwa kweli, hakuna mwingine katika ulimwengu wote ambaye anatumainika zaidi kuliko Baba yetu mpendwa wa mbinguni. Hata hivyo, ingawa ni rahisi kusoma maneno haya katika kitabu cha Mithali, huenda isiwe rahisi kuyatenda.
19 Wengi wana maoni yasiyofaa kuhusu maana ya kumtumaini Yehova. Wengine hufikiri kwamba kumtumaini Yehova kunamaanisha kuwa na hisia fulani yenye kufurahisha ambayo huchemka moyoni mwao. Huenda wengine wakafikiri kumtumaini Mungu humaanisha kwamba tunaweza kutarajia atukinge na taabu zote, atatue matatizo yetu yote, na atuondolee majaribu yetu mara moja kama tunavyotaka! Lakini maoni hayo hayana msingi. Kuwa na tumaini kunahusisha mengi zaidi kuliko kuwa na hisia fulani, na si jambo la kuwaziwa tu. Kwa watu wazima, kuwa na tumaini kunahusisha kufanya maamuzi baada ya kuyafikiria kwa makini.
20, 21. Kumtumaini Yehova kunahusisha nini? Toa mfano.
20 Ona tena jinsi Mithali 3:5 inavyosema. Inatofautisha kumtumaini Yehova na kutegemea akili zetu wenyewe, ikionyesha kwamba hatuwezi kufanya yote mawili. Je, hiyo inamaanisha kwamba haturuhusiwi kutumia nguvu zetu za uelewevu? La, kwa kuwa Yehova ndiye aliyetupa nguvu hizo na anatarajia tuzitumie kumtumikia. (Waroma 12:1) Lakini sisi hutegemea nini? Ikiwa kufikiri kwetu hakupatani na kwa Yehova, je, sisi tunakubali kwamba hekima yake ni ya juu sana kuliko yetu? (Isaya 55:8, 9) Kumtumaini Yehova humaanisha kuacha kufikiri kwake kuongoze kufikiri kwetu.
21 Kwa mfano: Wazia mtoto mdogo akiwa ameketi kwenye kiti cha nyuma cha gari huku wazazi wake wakiwa mbele. Baba yake ndiye anayeendesha gari hilo. Matatizo yakitokea wakati wa safari, labda kuhusu barabara inayofaa au hali ya hewa au hali ya barabara, mtoto mtiifu na mwenye kutumaini wazazi atatendaje? Je, atawaamuru la kufanya, akimwambia baba yake jinsi ya kuendesha gari? Je, atatilia shaka uamuzi wa wazazi wake au akatae kusikiliza anapoambiwa aendelee kuketi akiwa amejifunga mkanda wa usalama? La, kwa kawaida yeye atawatumaini wazazi wake washughulikie mambo hayo hata ingawa wao si wakamilifu. Yehova ni Baba yetu mkamilifu. Je, hatupaswi kumtumaini kabisa, hasa tunapokabili hali ngumu?—Isaya 30:21.
-