Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unatimiza Wajibu Wako Wote kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • Wajibu Wetu Wote kwa Mungu

      15. (a) Unaweza kuelezaje maneno ya Solomoni kuhusu “wajibu wote wa mwanadamu”? (b) Ni lazima tufanye nini ili tutimize wajibu wetu kwa Mungu?

      15 Akijumlisha uchunguzi wake wote, mhubiri, Solomoni, asema: “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu [“ndiyo wajibu wote wa mwanadamu,” NW].

  • Je, Unatimiza Wajibu Wako Wote kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • (Mhubiri 12:13, 14) Kumcha au kumstahi Muumba wetu Mtukufu kwa njia ifaayo, kutatulinda, na twatumaini kutalinda familia zetu pia, tusifuate mwenendo wa kipumbavu wa maisha ambao unaweza kutuletea sisi na wapendwa wetu matatizo mengi na huzuni nyingi. Kicho kifaacho cha Mungu ni safi na ndicho mwanzo wa hekima na ujuzi. (Zaburi 19:9; Mithali 1:7) Tukiwa na ufahamu wa ndani wa Neno la Mungu lililopuliziwa na kutumia mashauri yake katika mambo yote, tutatimiza “wajibu [wetu] wote” kwa Mungu. Kufanya hivyo hakumaanishi kuorodhesha wajibu mbalimbali. Badala yake, inatakikana tuchunguze Maandiko tunapotatua matatizo ya maisha na sikuzote kufanya mambo kwa njia ya Mungu.

  • Je, Unatimiza Wajibu Wako Wote kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
    • Lakini kichocheo kikubwa zaidi chapaswa kuwa upendo wetu kwa Baba yetu wa kimbingu, kwa kuwa mtume Yohana aliandika: “Kwa maana hivi ndivyo kumpenda Mungu humaanisha, kwamba tushike amri zake; na bado amri zake si zenye kulemea.” (1 Yohana 5:3) Na kwa kuwa amri za Mungu zimekusudiwa ziendeleze hali-njema yetu ya milele, kwa hakika ni jambo linalofaa na hata lenye hekima kuzitimiza. Huo si mzigo kwa wapendao Muumba Mtukufu. Wanataka kutimiza wajibu wao kwake.

      Timiza Wajibu Wako Wote

      17. Tutafanya nini ikiwa kwa kweli tunataka kutimiza wajibu wetu wote kwa Mungu?

      17 Ikiwa sisi ni wenye hekima na kwa kweli tunatamani kutimiza wajibu wetu wote kwa Mungu, mbali na kuzishika amri zake, tutakuwa na hofu yenye staha ya kutompendeza. Kwa kweli, “kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,” na wale wanaozishika amri zake wana “akili njema.” (Zaburi 111:10; Mithali 1:7) Basi na tuendelee kutenda kwa hekima na kumtii Yehova katika mambo yote. Na ni muhimu sana sasa kufanya hivyo, kwa kuwa Mfalme Yesu Kristo yupo, na siku yake ya hukumu akiwa Hakimu aliyewekwa na Mungu imekaribia.—Mathayo 24:3; 25:31, 32.

      18. Tutapata matokeo gani tukitimiza wajibu wetu wote kwa Yehova Mungu?

      18 Kila mmoja wetu sasa anachunguzwa na Mungu. Je, tuna mtazamo wa kiroho, ama tumeruhusu uvutano wa kilimwengu udhoofishe uhusiano wetu pamoja na Mungu? (1 Wakorintho 2:10-16; 1 Yohana 2:15-17) Tuwe vijana au wazee, na tufanye yote tuwezayo ili tumpendeze Muumba wetu Mtukufu. Tukimtii Yehova na kuzishika amri zake, tutakataa mambo ya ubatili ya ulimwengu huu wa kale unaopitilia mbali. Ndipo tunapoweza kuwa na tumaini la uhai udumuo milele katika mfumo mpya wa Mungu ambao aliahidi. (2 Petro 3:13) Hayo ni matazamio mazuri ajabu kama nini kwa wale wote wanaotimiza wajibu wao wote kwa Mungu!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki