-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
2. Mwanamke fulani aliyelala gizani anapewa amri gani, na kwa nini anapaswa kutii haraka?
2 Maneno ya kwanza ya sura hii ya Isaya yameelekezwa kwa mwanamke mwenye hali za huzuni. Ni wazi kwamba mwanamke huyo amelala kifudifudi gizani. Kwa ghafula, nuru yapenya ule weusi, huku Yehova akimtumia Isaya kupaaza sauti hivi: “Ondoka, [“inuka, Ee mwanamke,” “NW”] uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja; na utukufu wa BWANA umekuzukia.” (Isaya 60:1) Ndiyo, “mwanamke” huyo anapaswa kusimama ili yeye naye aangaze utukufu wa Mungu!
-
-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ni lazima “mwanamke” huyo ‘aangaze’ kwa faida ya wale wanaomzunguka, ambao wangali wanapapasa-papasa gizani.
-
-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
3. (a) “Mwanamke” huyo ni nani? (b) Kwa nini “mwanamke” huyo amekuwa akilala gizani?
3 Ingawa Yehova anaongea juu ya matukio ya wakati ujao, anamwambia yule “mwanamke” kwamba nuru yake “imekuja.” Hiyo inakazia uhakika wa kwamba unabii huo utatimizwa. “Mwanamke” anayetajwa ni Sayuni, au Yerusalemu, jiji kuu la Yuda. (Isaya 52:1, 2; 60:14) Jiji hilo linawakilisha taifa zima. Wakati wa utimizo wa kwanza wa unabii huo, “mwanamke” huyo anapatikana amelala gizani, na amekuwa hapo tangu Yerusalemu lilipoharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. Hata hivyo, mwaka wa 537 K.W.K., mabaki waaminifu kati ya Wayahudi waliohamishwa wanarudi Yerusalemu na kurudisha ibada safi. Mwishowe, Yehova anaangaza nuru juu ya “mwanamke” wake, na watu wake waliorudishwa wanakuwa chanzo cha kuangaza nuru miongoni mwa mataifa yaliyo katika giza la kiroho.
Utimizo Mkubwa Zaidi
4. Ni akina nani leo duniani wanaowakilisha yule “mwanamke,” na matumizi mapana ya unabii huo yanahusu nani?
4 Licha ya kupendezwa na utimizo wa unabii huu kuhusiana na Yerusalemu la kale, tunapendezwa pia na utimizo wake wa baadaye. Leo “mwanamke” wa kimbingu wa Yehova anawakilishwa duniani na “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Katika muda ambao taifa hili la kiroho limekuwako, tangu Pentekoste 33 W.K. mpaka sasa, limekuja kuwa na jumla ya washirika watiwa-mafuta 144,000, “ambao wamenunuliwa kutoka katika dunia” wakitazamia kutawala pamoja na Kristo mbinguni. (Ufunuo 14:1, 3) Utimizo wa kisasa wa Isaya sura ya 60 unawahusu hasa wale 144,000 walio hai duniani wakati wa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Unabii huu unawahusu pia waandamani wa Wakristo hao watiwa-mafuta, yaani “umati mkubwa” wa “kondoo wengine.”—Ufunuo 7:9; Yohana 10:11, 16.
5. Washiriki waliobaki wa Israeli wa Mungu walijikuta wakiwa wamelala gizani lini, na nuru ya Yehova iliwaangazia lini?
5 Kwa muda mfupi katika miaka ya mapema ya 1900, washirika wa Israeli wa Mungu ambao wangali duniani walikuwa wakisujudu gizani, kwa usemi wa mfano. Vita ya kwanza ya ulimwengu ilipokuwa ikikaribia kumalizika, walikuwa katika hali inayoelezwa kwa njia ya mfano katika kitabu cha Ufunuo, yaani, maiti zao zilikuwa zimelala “juu ya njia pana ya jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho laitwa Sodoma na Misri.” (Ufunuo 11:8) Hata hivyo, mwaka wa 1919 Yehova akawaangazia nuru yake. Nao wakaitikia kwa kusimama na kuangazia wengine nuru hiyo, wakitangaza habari njema za Ufalme wa Mungu bila hofu.—Mathayo 5:14-16; 24:14.
-