-
Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa NuruMnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
-
-
Wakati umewadia kwa mwanamke huyo kusimama ili aangaze nuru ya Mungu, yaani, utukufu wake. Kwa nini? Tunapata jibu katika mstari unaofuata: “Tazama, giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu; bali BWANA atakuzukia wewe, na utukufu wake utaonekana juu yako.” (Isaya 60:2)
-
-
Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa NuruMnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
-
-
5 Maneno yenye kusisimua yaliyo katika mistari hii mitatu ni utangulizi wa Isaya sura ya 60 na vilevile muhtasari wa mambo makuu ya sura hiyo. Sura hiyo inatabiri yale yatakayompata yule mwanamke wa kiunabii, na inaeleza jinsi tunavyoweza kukaa katika nuru ya Yehova licha ya giza linalofunika wanadamu. Lakini mifano inayotajwa katika mistari hiyo mitatu ya utangulizi inamaanisha nini?
6. Mwanamke anayetajwa katika sura ya 60 ya Isaya ni nani, naye anawakilishwa na nani duniani?
6 Mwanamke anayetajwa katika Isaya 60:1-3 ni Sayuni, tengenezo la kimbingu la Yehova la viumbe wa roho. Leo, Sayuni anawakilishwa duniani na mabaki ya “Israeli wa Mungu,” lile kutaniko la kimataifa la Wakristo ambao wametiwa mafuta kwa roho. Wao wana tumaini la kutawala pamoja na Kristo mbinguni. (Wagalatia 6:16) Taifa hilo la kiroho lina washiriki 144,000, na utimizo wa kisasa wa Isaya sura ya 60 unahusu hasa wale walio hai duniani katika “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1; Ufunuo 14:1)
-
-
Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa NuruMnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
-
-
7. Hali ya Sayuni ilikuwaje mwaka wa 1918, na hali hiyo ilikuwa imetabiriwa jinsi gani?
7 Je, “Israeli wa Mungu” alikuwa amelala gizani wakati fulani, kama yule mwanamke wa kiunabii? Ndiyo, jambo hilo lilitukia zaidi ya miaka 80 iliyopita. Wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu, Wakristo watiwa-mafuta walijitahidi sana kuendeleza kazi ya kutoa ushahidi. Lakini mwaka wa 1918, mwaka wa mwisho wa vita, kazi ya kuhubiri karibu ikomeshwe kabisa. Joseph F. Rutherford, aliyesimamia kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote, na Wakristo wengine mashuhuri walihukumiwa vifungo virefu gerezani kwa mashtaka bandia. Katika kitabu cha Ufunuo, Wakristo watiwa-mafuta waliokuwa duniani wakati huo walitajwa katika unabii huo kuwa maiti zilizolala “juu ya njia pana ya jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho laitwa Sodoma na Misri.” (Ufunuo 11:8) Kwa kweli huo ulikuwa wakati wenye giza kwa Sayuni aliyewakilishwa na watoto wake watiwa-mafuta duniani.
8. Ni badiliko gani kubwa lililotukia mwaka wa 1919, na matokeo yalikuwa nini?
8 Hata hivyo, mwaka wa 1919 kukawa na badiliko kubwa. Yehova aliangaza nuru juu ya Sayuni! Washiriki wa Israeli wa Mungu waliokuwa duniani walianza kuangaza nuru ya Mungu, wakaanza tena kuzitangaza habari njema kwa ujasiri. (Mathayo 5:14-16)
-