Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa Nuru
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
    • 12 Si wafanyabiashara peke yao walio safarini. Wachungaji wengi wanamwendea Sayuni pia. Unabii unasema hivi: “Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako, kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia.” (Isaya 60:7a) Makabila yanayofuga mifugo yanakuja hadi jiji takatifu ili kumtolea Yehova wanyama bora kutoka katika makundi yao. Hata wanajitoa kumtumikia Sayuni! Yehova anawakaribishaje wageni hao? Mungu mwenyewe anajibu hivi: “Watapanda juu ya madhabahu yangu kwa kibali, nami nitaitukuza [“nitairemba,” NW] nyumba ya utukufu wangu.” (Isaya 60:7b) Yehova anakubali kwa fadhili matoleo na utumishi wa wageni hao. Wanaliremba hekalu lake.

  • Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa Nuru
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
    • Hata hivyo, je, uliona kwamba mstari wa 7 unasema kwamba wapya hao wanaowasili ‘hupanda juu ya madhabahu ya Mungu’? Madhabahu ni mahali pa kutolea dhabihu, na maneno hayo ya unabii yanatukumbusha kwamba kumtumikia Yehova kunahusisha kujidhabihu. Mtume Paulo aliandika hivi: “Nawasihi sana . . . mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri kuzuri.” (Waroma 12:1) Kwa kupatana na maneno ya Paulo, Wakristo wa kweli hawatosheki tu kwenda kumwabudu Mungu mara moja kwa juma. Wanatumia wakati wao, nguvu na mali zao ili kuendeleza ibada safi. Je, waabudu hao wanaojitoa, wanairemba nyumba ya Yehova? Unabii wa Isaya unajibu, ndiyo. Na tunaweza kuwa na uhakika kwamba waabudu hao wenye bidii pia wamerembwa vizuri machoni pa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki