Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni Pote
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 29, 30. “Mdogo” amekuwaje “elfu”?

      29 Mwishoni mwa Isaya sura ya 60 mnaweza kupatikana ahadi nzito, ambayo Yehova anaitoa kwa kutumia jina lake mwenyewe kuhakikisha kabisa kwamba ataitimiza. Anasema hivi: “Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa hodari; mimi, BWANA, nitayahimiza hayo wakati wake.” (Isaya 60:22) Wakati watiwa-mafuta waliotawanywa waliporudishwa kwenye utendaji mwaka wa 1919, wao ndio waliokuwa yule “mdogo.”e Lakini idadi yao iliongezeka wakati Waisraeli wa kiroho waliobaki walipokuwa wakiletwa ndani. Kisha ongezeko hilo likawa kubwa sana wakati umati mkubwa ulipoanza kukusanywa.

      30 Muda si muda, amani na uadilifu uliomo miongoni mwa watu wa Mungu ukawavutia watu wengi sana wenye mioyo ya kupenda haki kiasi cha kwamba yule “mdogo” akaongezeka kuwa “taifa hodari” kihalisi. Kwa sasa taifa hilo lina watu wengi kuliko mataifa mengi ya ulimwengu yanayojitawala. Ni wazi kwamba Yehova, kupitia Yesu Kristo, ameelekeza kazi ya Ufalme na kuihimiza. Kuona ibada ya kweli ikipanuka ulimwenguni pote na kushiriki katika mpanuko huo kunasisimua kama nini! Ndiyo, ni shangwe kutambua kwamba ongezeko hili humletea Yehova utukufu, aliyetoa unabii wa mambo hayo zamani za kale.

  • Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni Pote
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • e Mwaka wa 1918 idadi ya wastani ya wale walioshiriki kulihubiri neno kila mwezi ilikuwa ndogo kuliko 4,000.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki