-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Sasa Yehova anatumia mfano tofauti na kuongea na watu wake kana kwamba anaongea na jiji lenye kuta: “Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha [“kumtaja,” “NW”] BWANA, msiwe na kimya;
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Mchana na usiku, walinzi katika kuta hizo wako macho kuhakikisha kwamba jiji lina usalama, na kuwapasha wakaaji wake habari za kuwaonya.—Nehemia 6:15; 7:3; Isaya 52:8.
14 Nyakati za kisasa Yehova amewatumia walinzi wake watiwa-mafuta kuwaonyesha watu watiifu njia ya kupata uhuru kutoka kwenye utumwa wa dini ya uwongo. Watu hao wamealikwa waje ndani ya tengenezo lake, ambamo wanalindwa wasipatwe na uchafu wa kiroho, mavutano ya kutomhofu Mungu, na ili wasichukiwe na Yehova. (Yeremia 33:9; Sefania 3:19) Jamii ya mlinzi, yaani yule “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” inatimiza fungu muhimu sana la kutoa ulinzi huo, kwani inaandaa ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao.’ (Mathayo 24:45-47)
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
15. Jamii ya mlinzi na waandamani wao wanamtumikiaje Yehova daima?
15 Jamii ya mlinzi na waandamani wake inaendelea kutoa utumishi! Mtazamo wao wa kujitoa kwa nafsi yote unaonekana katika utendaji wenye bidii unaofanywa na mamilioni ya watu mmoja-mmoja walio waaminifu, huku wakiungwa mkono na waangalizi wanaosafiri na wake zao; watu waliojitolea katika makao mbalimbali ya Betheli na katika sehemu za uchapaji za Mashahidi wa Yehova; mishonari; na mapainia wa pekee, wa kawaida, na wasaidizi. Zaidi ya hilo, wanajibidiisha kujenga Majumba mapya ya Ufalme, kutembelea wagonjwa, kusaidia watu mmoja-mmoja wanaokabili hali ngumu za kitiba, na kuwapa msaada wa wakati wake wale wanaopatwa na majanga na misiba. Mara nyingi, wengi wa watu hawa wenye kujidhabihu hutumikia kihalisi “mchana na usiku”!—Ufunuo 7:14, 15.
-