-
Yehova Ajifanyia Jina MaridadiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Fadhili za Upendo wa Mungu
14. Sasa Isaya anatoa vikumbusha gani vinavyofaa?
14 Nyakati zilizopita, Wayahudi waliacha upesi kuyathamini mambo ambayo Yehova aliwafanyia. Basi, inafaa kwamba Isaya anawakumbusha ni kwa nini Yehova alifanya mambo hayo. Isaya anatangaza hivi: “Nitautaja wema wa BWANA, sifa za BWANA kwa yote aliyotukirimia BWANA; na wingi wa wema wake kwa nyumba ya Israeli, aliowakirimia kwa rehema zake, na kwa wingi wa wema [“fadhili za upendo,” “NW”] wake.
-
-
Yehova Ajifanyia Jina MaridadiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
15. Yehova aliwaonyeshaje wazao wa Abrahamu fadhili za upendo kule Misri, na kwa nini alifanya hivyo?
15 Yehova anaweka mfano wa kutokeza kama nini kwa kuonyesha fadhili za upendo, au upendo wenye uaminifu-mshikamanifu! (Zaburi 36:7; 62:12) Yehova alishikamana na Abrahamu kwa njia yenye upendo. (Mika 7:20) Alimwahidi mzee huyo wa ukoo kwamba mataifa yote ya dunia yangejibariki kupitia mbegu yake, au uzao wake. (Mwanzo 22:17, 18) Yehova alishikamana na ahadi hiyo, akaionyesha nyumba ya Israeli wema tele. Mojawapo la matendo yake ya uaminifu-mshikamanifu yenye kutokeza lilikuwa lile la kuwaokoa wazao wa Abrahamu kutoka utumwani Misri.—Kutoka 14:30.
-