Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ajifanyia Jina Maridadi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Kama ng’ombe wapelekwavyo malishoni bondeni, ndivyo roho ya Mungu ilivyowapumzisha watu wake.”—Isaya 63:11-14a, “BHN.”d

  • Yehova Ajifanyia Jina Maridadi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Baada ya muda, Mungu aliwaondoa katika lile jangwa kubwa la kuogofya, akawaongoza kuwaingiza nchi inayotiririka maziwa na asali—mahali pa pumziko. (Kumbukumbu la Torati 1:19; Yoshua 5:6; 22:4) Ingawa hivyo, sasa Waisraeli wanateseka kwa sababu wamepoteza uhusiano wao mzuri na Mungu!

      ‘Ajifanyia Jina Maridadi’

      21. (a) Israeli angaliweza kuwa na pendeleo gani kuu kuhusiana na jina la Mungu? (b) Ni sababu gani ya msingi iliyofanya Mungu awakomboe wazao wa Abrahamu kutoka Misri?

      21 Na bado, hasara ya vitu vya kimwili inayowapata Waisraeli ni kitu kidogo sana ikilinganishwa na hasara ya pendeleo ambalo wametupa, yaani, kushiriki kulitukuza jina la Mungu. Musa aliwaahidi Waisraeli hivi: “BWANA atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya BWANA, Mungu wako, na kutembea katika njia zake. Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la BWANA, nao watakuwa na hofu kwako.” (Kumbukumbu la Torati 28:9, 10) Wakati Yehova alipochukua hatua ya kuwalinda wazao wa Abrahamu, akiwaokoa utumwani Misri, hakuwa akifanya hivyo ili kurahisisha tu maisha yao au kuyafanya yawe ya kupendeza zaidi. Alikuwa akichukua hatua kwa ajili ya jambo la maana zaidi sana—jina lake. Naam, alitaka kuhakikisha kwamba jina lake ‘linatangazwa katika dunia yote.’ (Kutoka 9:15, 16) Na wakati Mungu alipoonyesha rehema baada ya ule uasi wa jangwani, hakufanya hivyo kwa msisimuko tu. Yehova mwenyewe alisema hivi: “Nalitenda kwa ajili ya jina langu, ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa.”—Ezekieli 20:8-10.

      22. (a) Katika wakati ujao, kwa nini Mungu atawapigania watu wake tena? (b) Upendo wetu kwa jina la Mungu una matokeo gani juu ya vitendo vyetu?

      22 Kisha Isaya anaupa unabii huu umalizio wenye nguvu kama nini! Anasema hivi: “Ndivyo ulivyowaongoza watu wako, ili ujifanyie jina lenye utukufu [“lililo maridadi,” “NW”].” (Isaya 63:14b) Sasa inaweza kuonekana wazi ni kwa nini Yehova anapigania masilahi ya watu wake kwa nguvu nyingi sana. Kusudi lake ni kujifanyia jina lililo maridadi. Hivyo, unabii wa Isaya ni kikumbusha cha kwamba kubeba jina la Yehova ni pendeleo la kuogopesha sana na pia ni daraka kubwa. Wakristo wa kweli leo wanalipenda jina la Yehova kuliko uhai wao wenyewe. (Isaya 56:6; Waebrania 6:10) Wanachukia sana kufanya jambo lolote ambalo lingeweza kuliletea suto jina hilo takatifu. Wanauitikia upendo wa Mungu wenye uaminifu-mshikamanifu kwa kushikamana naye kwa uaminifu. Na kwa sababu wanalipenda jina maridadi la Yehova, wanatamani sana kuiona siku ambayo atawakanyaga-kanyaga adui zake katika shinikizo la divai la hasira yake—si kwa sababu wao tu watafaidika, bali kwa sababu jina la Mungu huyu wampendaye litatukuzwa.—Mathayo 6:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki