Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.” (Isaya 65:3-5)

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 8 Kwa kweli, watenda-dhambi hao wanaojiona kuwa waadilifu ni kama wanawaambia hivi Wayahudi wenzao: ‘Kaa mbali nami, kwa sababu mimi ni mtakatifu kukushinda.’ Unafiki gani huo!

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Hata hivyo, utendaji wao wa kidini unawafanya wajione kuwa watakatifu kuliko Wayahudi wengine, na wanataka wengine wakae mbali nao, eti watu hao wasitakasike au kuwa safi kwa sababu ya kushirikiana nao. Hata hivyo, jambo hilo halipatani hata kidogo na maoni ya yule Mungu ambaye hutaka apewe “ujitoaji wa pekee”!—Kumbukumbu la Torati 4:24, NW.

      9. Yehova anawaonaje watenda-dhambi hao wanaojiona kuwa waadilifu?

      9 Badala ya kuwaona kuwa watakatifu watu hawa wanaojiona kuwa waadilifu, Yehova anasema hivi: “Watu hao ni moshi puani mwangu.” Neno la Kiebrania la kutaja ‘pua’ au ‘tundu la pua’ hutumiwa mara nyingi kwa njia ya mfano kumaanisha hasira. Vilevile, moshi hushirikishwa na hasira ya Yehova inayowaka. (Kumbukumbu la Torati 29:20) Ibada ya sanamu yenye kuchukiza ambamo watu wake wametumbukia imechochea hasira kali ya Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki