-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
14 Yehova anawaonya wazi hivi: “Mimi nitawaandikia [“nitawajalia,” “NW”] kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa; kwa sababu nilipoita hamkuitika; niliponena, hamkusikia; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia.” (Isaya 65:12) Kwa kutumia Kiebrania cha awali, Yehova anagonganisha maneno ‘jalia’ na “ajali” kusema kwamba wale wanaomwabudu mungu huyo wa uwongo ‘watajaliwa kuuawa kwa upanga,’ maana yake kupatwa na uharibifu. Mara nyingi Yehova amewatumia manabii wake kuwahimiza watu hao watubu, lakini wamempuuza wakaamua kwa vichwa vigumu kufanya yale wanayojua ni mabaya machoni pake. Lo, wanamwonyesha Mungu madharau yaliyoje! Onyo la Mungu litatimizwa wakati taifa hilo litakapopatwa na maangamizi makubwa mwaka wa 607 K.W.K. Huo ni wakati ambao Yehova atawaruhusu Wababiloni waharibu Yerusalemu na hekalu lake. Hapo “mungu wa Bahati Nzuri” atashindwa kuwalinda wafuasi wake wenye bidii walioko Yuda na Yerusalemu.—2 Mambo ya Nyakati 36:17.
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Wanasadiki kwamba wale wanaojitoa kufanya mapenzi ya mungu huyo watapoteza kila kitu hatimaye, kwani Yehova anawaambia hivi watu wa namna hiyo: ‘Nitawajalia kuuawa kwa upanga.’
-