-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ahadi ya Wakati Ujao Wenye Usalama
27. Isaya anaelezaje kuhusu usalama ambao wale wenye kurudi wataufurahia katika nchi yao?
27 Katika utimizo wa kwanza, maisha yatakuwaje kwa Wayahudi wenye kurudi wakiwa chini ya mbingu mpya? Yehova anasema hivi: “Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.” (Isaya 65:20) Hiyo inaonyesha vizuri kama nini usalama ambao wahamishwa wenye kurudi watafurahia katika nchi yao iliyorudishwa! Kifo kisichotazamiwa hakitampata mzaliwa-juzi, maana yake kitoto cha siku chache tu. Wala kifo cha jinsi hiyo hakitammaliza mzee asiyetimiza maisha yake.d Maneno ya Isaya yanawafariji kweli kweli Wayahudi watakaorudi Yuda! Wakiisha kuwa salama nchini mwao, hawana tena haja ya kufanya wasiwasi eti adui zao watasomba watoto wao wachanga au kuchinja mashujaa wao.
28. Tunajifunza nini kutokana na maneno ya Yehova juu ya maisha katika ulimwengu mpya chini ya Ufalme wake?
28 Maneno ya Yehova yanatuambia nini juu ya maisha katika ulimwengu mpya unaokuja? Chini ya Ufalme wa Mungu, kila mtoto atakuwa na tarajio la kupata wakati ujao ulio salama. Kifo hakitaua tena mwanamume anayemhofu Mungu akiwa katika umri wake wa ufanisi mkubwa. Bali, wanadamu watiifu watakuwa salama salimini, na wataweza kufurahia maisha. Namna gani watu wowote wanaochagua kumwasi Mungu? Watapoteza pendeleo la uhai. Hata ikiwa mtenda-dhambi anayeasi ana “umri wa miaka mia,” atakufa. Hapo yeye atakuwa “mtoto wa siku chache” akilinganishwa na vile angaliweza kuwa—mtu mwenye maisha yasiyo na kikomo.
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Biblia iitwayo The Jerusalem Bible hufasiri Isaya 65:20 hivi: “Hakutapatikana tena kitoto kichanga chenye kuishi siku chache tu, wala mzee asiyeishi hadi mwisho wa siku zake.”
-