Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nuru kwa Mataifa
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Sanduku katika ukurasa wa 409]

      Zawadi Zilizotiwa Mafuta za Kumpa Yehova Kutoka Katika Mataifa Yote

      Mwaka wa 1920, Juan Muñiz aliondoka Marekani kwenda Hispania kisha akasonga mbele na safari yake hadi Argentina, ambako aliyapanga kitengenezo makutaniko ya watiwa-mafuta. Kuanzia mwaka wa 1923 na kuendelea, nuru ya kweli iling’aa juu ya wenye mioyo minyoofu katika Afrika Magharibi wakati mishonari William R. Brown (ambaye mara nyingi aliitwa Bible Brown) aliposhika njia kwenda kuhubiri ujumbe wa Ufalme katika sehemu kama vile Sierra Leone, Ghana, Liberia, Gambia, na Nigeria. Mwaka huo huo George Young wa Kanada aliteremka Brazil, kisha akasonga mbele kwenda Argentina, Costa Rica, Panama, Venezuela, na hata Muungano wa Sovieti. Karibu na wakati huo huo, Edwin Skinner alisafiri baharini kutoka Uingereza hadi India, na huko akajikakamua muda wa miaka mingi katika kazi ya mavuno.

  • Nuru kwa Mataifa
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • ‘Kumletea Yehova Zawadi’

      12, 13. Kuanzia mwaka wa 537 K.W.K., “ndugu” wataletwa Yerusalemu kwa njia gani?

      12 Baada ya Yerusalemu kujengwa upya, Wayahudi waliotawanyika mbali sana na nchi yao wataelekeza fikira na mtazamo wao kwenye jiji hilo pamoja na ukuhani wake uliorudishwa likiwa kituo cha ibada safi. Wengi wao watasafiri mbali kuhudhuria sherehe za kila mwaka huko. Isaya anaandika hivi kwa kupuliziwa: “Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka [“zawadi,” “NW”] kwa BWANA, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema BWANA; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka [“zawadi,” “NW”] yao nyumbani kwa BWANA katika chombo safi. Na baadhi ya hao nitawatwaa kuwa makuhani na Walawi.”—Isaya 66:20, 21.

      13 Wengine wa hao ‘ndugu kutoka mataifa yote’ walikuwako siku ya Pentekoste wakati roho takatifu ilipomiminwa juu ya wanafunzi wa Yesu. Masimulizi hayo yanasema hivi: “Kulikuwa na Wayahudi wakikaa katika Yerusalemu, wanaume wenye kumhofu Mungu, kutoka kila taifa la yale yaliyo chini ya mbingu.” (Matendo 2:5) Walikuja Yerusalemu kuabudu kulingana na desturi ya Kiyahudi, lakini walipozisikia habari njema juu ya Yesu Kristo, wengi walionyesha wazi kwamba wanamwamini kisha wakabatizwa.

      14, 15. (a) Wakristo watiwa-mafuta waliwakusanyaje wengi wa “ndugu” zao wa kiroho baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, nao waliletwaje kwa Yehova wakiwa ‘zawadi katika chombo safi’? (b) Yehova ‘alitwaa baadhi ya hao kuwa makuhani’ jinsi gani? (c) Ni akina nani waliokuwa baadhi ya Wakristo watiwa-mafuta waliohusika katika kukusanya ndugu zao wa kiroho? (Ona sanduku katika ukurasa huu.)

      14 Je, unabii huu una utimizo wa kisasa? Tena sana. Baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, watumishi watiwa-mafuta wa Yehova walitambua kutokana na Maandiko kwamba Ufalme wa Mungu ulikuwa umeanzishwa mbinguni mwaka wa 1914. Kupitia funzo la uangalifu la Biblia, walijifunza kwamba warithi wa ziada wa Ufalme, au akina “ndugu,” walipasa kukusanywa. Wahudumu hodari walisafiri “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia,” wakitumia usafiri wa kila namna ili kuwatafuta wale waliotazamiwa kuwa washirika wa mabaki-watiwa mafuta, wengi wao wakitoka kwenye makanisa ya Jumuiya ya Wakristo. Walipopatikana, waliletwa wawe zawadi kwa Yehova.—Matendo 1:8.

      15 Watiwa-mafuta waliokusanywa miaka ya mapema hawakumtazamia Yehova awakubali wakiwa na hali waliyokuwa nayo kabla ya kuujua ukweli wa Biblia. Walichukua hatua za kujisafisha uchafu wa kiroho na wa kiadili ili waweze kutolewa wawe ‘zawadi katika chombo safi,’ au kama ilivyotajwa na mtume Paulo, wawe “bikira safi kiadili kwa Kristo.” (2 Wakorintho 11:2) Zaidi ya kukataa kosa la kimafundisho, watiwa-mafuta walilazimika kujifunza jinsi ya kudumisha msimamo wa kutokuwamo kabisa katika mambo ya kisiasa ya ulimwengu huu. Mwaka wa 1931, watumishi wake walipokuwa wamesafishwa kwa kiasi kinachofaa, Yehova aliwaonyesha neema kwa kuwapa pendeleo la kubeba jina lake wakiwa Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10-12)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki