-
Ahadi ya Mkuu wa AmaniUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Sheria na Ushuhuda” wa Mungu
8. Ni nini “sheria na ushuhuda” tunazopaswa kuziendea leo ili kupata mwelekezo?
8 Sheria ya Yehova inayopiga marufuku uwasiliani-roho, pamoja na amri zake nyingine, haijafichika katika Yuda. Imehifadhiwa kwa maandishi. Leo Neno lake lililokamilika lapatikana kwa maandishi. Neno hilo ni Biblia, ambayo ina mkusanyo wa sheria na kanuni za Mungu na vilevile masimulizi ya jinsi Mungu alivyoshughulika na watu. Masimulizi hayo ya Biblia ya shughuli za Yehova huandaa ushuhuda, au uthibitisho, unaotufundisha utu na sifa za Yehova. Badala ya kuwaendea wafu, Waisraeli wapaswa kutafuta mwelekezo kutoka wapi? Isaya ajibu: “Kwa sheria na ushuhuda”! (Isaya 8:20a) Naam, wale wanaotaka ujuzi wa kweli wapaswa kuligeukia Neno la Mungu lililoandikwa.
9. Je, watenda-dhambi wasiotubu watapata faida yoyote kwa kunukuu Biblia mara kwa mara?
9 Huenda baadhi ya Waisraeli wanaopendezwa na uwasiliani-roho wakadai kuwa wanalistahi Neno la Mungu lililoandikwa. Lakini hayo ni madai tu nayo ni ya kinafiki. Isaya asema: “Ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.” (Isaya 8:20b) Isaya arejezea neno gani hapa? Labda kwa neno: “Kwa sheria na ushuhuda.” Labda baadhi ya Waisraeli waasi-imani wanalirejezea Neno la Mungu, kama vile huenda waasi-imani na wengine leo wakanukuu Andiko. Lakini hayo ni maneno matupu tu. Kunukuu Andiko hakutatokeza “asubuhi [“nuru ya alfajiri,” NW],” au nuru ya Yehova, iwapo hakuandamani na kutenda mapenzi ya Yehova na kukataa mazoea yasiyo safi.b
-
-
Ahadi ya Mkuu wa AmaniUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
b Usemi, “neno hili” katika Isaya 8:20 labda warejezea neno linalohusu wawasiliani-roho, lililonukuliwa katika Isaya 8:19. Ikiwa ndivyo ilivyo, Isaya amaanisha kwamba watu wanaochangia kusitawi kwa uwasiliani-roho katika Yuda wataendelea kuwasihi wengine waende kwa wawasiliani-roho na hivyo wasipate nuru ya Yehova.
-