-
Yehova Anyenyekeza Jiji Lenye KujigambaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
3. (a) Ni nani “waliowekwa wakfu” ambao Yehova atainua? (b) Majeshi ya kipagani ‘yamewekwaje wakfu’?
3 Sasa Yehova asema: “Mimi mwenyewe nimewaamuru watu wangu waliowekwa wakfu kwangu, naam, nimewaita watu wangu walio hodari kwa ajili ya hasira yangu, watu wangu wenye kutakabari.
-
-
Yehova Anyenyekeza Jiji Lenye KujigambaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ni nani hao “waliowekwa wakfu” ambao wameteuliwa kuangusha jiji la Babiloni lenye kiburi? Ni majeshi ya mataifa yaliyoungana, “mataifa waliokutana pamoja.”
-
-
Yehova Anyenyekeza Jiji Lenye KujigambaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Wamewekwaje wakfu? Pasipo shaka si katika maana ya kuwa watakatifu. Hayo ni majeshi ya kipagani ambayo hayapendi hata kidogo kumtumikia Yehova. Hata hivyo, katika Maandiko ya Kiebrania, usemi “-liowekwa wakfu” humaanisha “-liotengwa ili kutumiwa na Mungu.” Yehova aweza kuweka wakfu majeshi ya mataifa na kutumia tamaa yao ya kujitakia makuu ili kudhihirisha hasira yake. Aliitumia Ashuru kwa njia hiyo. Ataitumia milki ya Babiloni vivyo hivyo. (Isaya 10:5; Yeremia 25:9) Naye atayatumia mataifa mengine kuadhibu Babiloni.
-