-
Mkono wa Yehova WainuliwaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
22. Watu wa Mungu wamebarikiwaje leo?
22 Katika utimizo wa leo, mabaki ya Israeli wa kiroho waliotiwa nidhamu waliachiliwa huru kutoka Babiloni Mkubwa nao wakarudishwa kwenye utumishi wa Yehova mwaka wa 1919. Huku wakiwa wametiwa nguvu upya, Wakristo watiwa-mafuta walijitolea kwa bidii kutimiza kazi yao ya kuhubiri. (Mathayo 24:14) Yehova naye amewabariki kwa kuwapa ongezeko, hata akauleta umati mkubwa wa “kondoo wengine” watumikie pamoja nao. (Yohana 10:16) “Umeliongeza hilo taifa, BWANA, umeliongeza taifa; wewe umetukuzwa, umeipanua mipaka yote ya nchi hii.
-