-
Isaya Atabiri ‘Tendo la Ajabu’ la YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
13. Ni nani aliye “jiwe lililojaribiwa,” na Jumuiya ya Wakristo imemkataaje?
13 Basi, viongozi hao wa kidini wapaswa kuwa wakitazama wapi? Isaya sasa arekodi ahadi ya Yehova: “Tazama, naweka jiwe katika Sayuni, liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani, msingi ulio imara; yeye aaminiye hatafanya haraka.
-
-
Isaya Atabiri ‘Tendo la Ajabu’ la YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Muda mfupi baada ya Isaya kuyasema maneno hayo, Mfalme Hezekia mwaminifu atawazwa huko Sayuni, na ufalme wake waokolewa, si kupitia kwa washirika jirani, bali kupitia kwa Yehova kuingilia kati. Hata hivyo, Hezekia siye anayeyatimiza maneno hayo yaliyopuliziwa. Mtume Petro, akinukuu maneno ya Isaya, alionyesha kuwa Yesu Kristo, mzao wa baadaye sana wa Hezekia, ndiye “jiwe lililojaribiwa” na yeyote anayedhihirisha imani katika Yeye hapaswi kuogopa kamwe. (1 Petro 2:6) Yachukiza sana kwa sababu viongozi wa Jumuiya ya Wakristo, wajapojiita Wakristo, wamefanya mambo ambayo Yesu alikataa kufanya! Wametafuta umashuhuri na mamlaka katika ulimwengu huu badala ya kumngojea Yehova alete Ufalme wake chini ya Yesu Kristo aliye Mfalme.—Mathayo 4:8-10.
-