-
Paradiso Yarudishwa!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Kuzaliwa kwa Taifa Jipya
19. Kwa nini twaweza kusema kwamba unabii wa Isaya una utimizo wa kiasi tu katika karne ya sita K.W.K.?
19 Hapana budi utimizo wa unabii wa Isaya sura ya 35 ni wa kiasi tu katika karne ya sita K.W.K. Hali za kiparadiso wanazofurahia Wayahudi waliorudishwa ni za muda tu. Baadaye, mafundisho ya kidini yasiyo ya kweli na uzalendo zachafua ibada safi. Wayahudi wapata tena huzuni na majonzi ya kiroho. Hatimaye Yehova awakataa wasiwe watu wake. (Mathayo 21:43) Furaha yao haidumu kwa sababu ya kutotii ambako kumetokea tena. Hayo yote yaonyesha kuwepo kwa utimizo mwingine ulio mkubwa zaidi wa Isaya sura ya 35.
20. Kulitokea Israeli gani jipya katika karne ya kwanza W.K.?
20 Kwa wakati wa Yehova uliowekwa, Israeli nyingine ya kiroho ilitokea. (Wagalatia 6:16) Yesu alitayarisha msingi wa kuzaliwa kwa hilo Israeli jipya wakati wa huduma yake duniani. Aliirudisha ibada safi, na maji ya ile kweli yakaanza kutiririka tena kupitia mafundisho yake.
-
-
Paradiso Yarudishwa!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
22. Wakristo waaminifu, waliotafuta kweli katika nyakati za kisasa waliingiaje kwenye utekwa wa Kibabiloni?
22 Namna gani leo? Je, unabii wa Isaya una utimizo mwingine, ulio kamili zaidi uhusuo kutaniko la Kikristo leo? Ndiyo. Baada ya mitume kufa, idadi ya Wakristo wa kweli ilipungua sana, na “magugu,” yaani Wakristo wasio wa kweli, yakasitawi duniani. (Mathayo 13:36-43; Matendo 20:30; 2 Petro 2:1-3) Hata wakati watu walio waaminifu katika karne ya 19 walipoanza kujitenga na Jumuiya ya Wakristo na kutafuta ibada safi, uelewevu wao bado ulichafuliwa na mafundisho yasiyopatana na Maandiko. Yesu alitawazwa kuwa Mfalme wa Kimesiya mwaka wa 1914, lakini muda mfupi baadaye, hali ya watu hao wenye kutafuta kweli kwa uaminifu ilionekana kuwa mbaya. Kama ilivyotabiriwa, mataifa ‘yalifanya vita pamoja nao na kuwashinda,’ na majaribio ya Wakristo hao waaminifu ya kuhubiri habari njema yakazimwa. Babiloni ikawateka.—Ufunuo 11:7, 8.
23, 24. Maneno ya Isaya yametimia kwa njia zipi miongoni mwa watu wa Mungu tangu mwaka wa 1919?
23 Hata hivyo, mambo yalibadilika mwaka wa 1919. Yehova aliwatoa watu wake utekwani. Walianza kuyakataa mafundisho yasiyo ya kweli yaliyochafua ibada yao hapo awali. Basi wakaponywa. Wakaingia katika paradiso ya kiroho, ambayo yaendelea kusambaa duniani kote hata sasa.
-
-
Paradiso Yarudishwa!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Jambo la maana zaidi ni kwamba wenye mioyo minyofu waliponyoka kutoka dini isiyo ya kweli nao wakaanza kufurahia paradiso ya kiroho katika kutaniko la Kikristo. (Isaya 52:11; 2 Wakorintho 6:17)
-