Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Paradiso Yarudishwa!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 9. Wayahudi wanaorudi watolewa ahadi gani tukufu?

      9 Wale waliowekwa huru kutoka utekwani Babiloni watakuwa na sababu nzuri ya kufurahi, kwa kuwa wakati ujao mtukufu unawangojea wanaporudi Yerusalemu. Isaya atabiri: “Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba.”—Isaya 35:5, 6a.

      10, 11. Ni kwa nini lazima maneno ya Isaya yawe na maana ya kiroho kwa Wayahudi wanaorudi, na maneno hayo yadokeza nini?

      10 Yaonekana Yehova aifikiria hali ya kiroho ya watu wake. Wameadhibiwa kwa kupelekwa uhamishoni kwa miaka 70 kwa sababu ya uasi wao wa awali. Hata hivyo, Yehova ajapowatia watu wake nidhamu, hakuwapiga kwa upofu, uziwi, ulemavu, na ububu. Basi, kurudisha taifa la Israeli hakuhitaji uponyaji wa kasoro za kimwili. Yehova arudisha kile kilichopotea, yaani, afya ya kiroho.

      11 Wayahudi wenye kutubu waponywa kwa kupata tena uwezo wao mbalimbali wa kiroho—uwezo wao wa kuona kiroho na uwezo wao wa kusikia, kutii, na kunena neno la Yehova. Wao watambua uhitaji wao wa kukaa karibu na Yehova. Kupitia mwenendo mzuri, ‘waimba’ kwa furaha ya kumsifu Mungu wao. Aliyekuwa “kilema” hapo awali apata hamu na nguvu ya kuabudu Yehova. “Ataruka-ruka kama kulungu” kitamathali.

  • Paradiso Yarudishwa!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Yehova Awaburudisha Watu Wake

      12. Yehova ataibariki nchi kwa maji kadiri gani?

      12 Ni vigumu kuwazia paradiso isiyo na maji. Paradiso ya kwanza huko Edeni ilikuwa na maji mengi. (Mwanzo 2:10-14) Nchi waliyopewa Israeli pia ilikuwa “nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo.” (Kumbukumbu la Torati 8:7) Kwa kufaa basi, Isaya atoa ahadi hii yenye kuburudisha: “Katika nyika maji yatabubujika; na vijito jangwani. Na mchanga ung’aao mfano wa maji utakuwa ziwa la maji, na nchi yenye kiu itakuwa chemchemi za maji; katika makao ya mbweha, walipokuwa wamelala, patakuwa na majani, pamoja na mianzi na manyasi.” (Isaya 35:6b, 7) Waisraeli watakapoanza kuitunza nchi tena, sehemu zenye ukiwa ambapo mbweha walikaa wakati fulani zitafunikwa kwa majani tele yanayonawiri na yenye rangi ya kijani. Nchi kame na yenye vumbi itageuzwa kuwa mahali penye “matope” panapoweza kumea mafunjo na mianzi mingine imeayo majini.—Ayubu 8:11.

      13. Taifa lililorudishwa litapewa maji gani mengi ya kiroho?

      13 Ingawa hivyo, jambo la maana zaidi ni yale maji ya kiroho ya ile kweli, ambayo Wayahudi waliorudishwa watapata kwa wingi. Yehova atatoa ujuzi, kitia-moyo, na faraja kupitia Neno lake. Na zaidi, wanaume na wakuu wazee waaminifu watakuwa “kama mito ya maji mahali pakavu.” (Isaya 32:1, 2) Wale wanaoendeleza ibada safi, kama vile Ezra, Hagai, Yoshua, Nehemia, Zekaria, Zerubabeli, kwa kweli watakuwa ushuhuda ulio hai wa utimizo wa unabii wa Isaya.—Ezra 5:1, 2; 7:6, 10; Nehemia 12:47.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki